Na Woinde Shizza, Michuzi Tv-Arusha
MKUU wa Mkoa wa Arusha,  Iddi Hassan Kimanta amemwagiza afisa elimu Mkoa, Halfan Omari Masukira kumvua madaraka ya ukuu wa shule mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Irkaswa, Arbogastus Mushi na mwalimu wa taaluma kwa kushindwa kusimamia ufundishaji katika shule hiyo iliyopo Wilayani Longido.

Maelekezo hayo ameyatoa alipokuwa akizungumza katika kikao na Maafisa Elimu kutoka katika Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha, Kikao kilichofanyika Katika ukumbi wa jengo la mkuu wa mkoa Arusha.

Kimanta amesema ni aibu kubwa sana kwa mwalimu mkuu kutohakikisha vipindi vyote vinafundishwa na walimu wake kwa wakati.

“Hii inaashiria ni usimamizi mbovu wa mwalimu mkuu na mwalimu wa taaluma, kwani wanafunzi wamekuwa wakifundishwa masomo machache kwa siku huku mwalimu mkuu hajui chochote.” Alisema.

Amewataka maafisa elimu hao kwenda kuwasimamia walimu wakuu wa shule kwa ukaribu zaidi, kwani Mkoa wa Arusha unasifa ya kushika nafasi nzuri katika matokea ya mitihani mbalimbali, hivyo baadhi ya walimu wakuu wasikwamishe jitihada hizo.

Nae, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Arusha David Lyimongi, amemuagiza Afisa Elimu mkoa, bwana Masukira kuhakikisha miongozo yote inayoletwa kutoka TAMISEMI iwe inaendana na uhalisia wa hali ya sasa ili sekta ya elimu iendelee kuimarika zaidi.

Mkoa wa Arusha umekuwa ukifanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa na kwa mwaka 2020 kidato cha sita Mkoa ulishika nafasi ya 7 Kitaifa, kidato cha nne nafasi ya 1, kidato cha pili nafasi ya 1, darasa la saba nafasi ya 2 na darasa la nne nafasi ya 3.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...