Na
Immaculate Makilika – MAELEZO
SERIKALI imeendelea kutambua maeneo yote yenye migogoro ya ardhi
ili kuitatua kwa lengo la kuondoa changamoto hiyo kwa wananchi.
Akijibu swali jana
Bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Elias
Kwandikwa alisema kuwa mgogoro wa ardhi
kati ya Kambi ya Jeshi ya Itaka na vijiji
vya Itewe na Sasenga vilivyopo jimbo la
Mbozi, pamoja na mgogoro wa ardhi wa Kasulu imesababishwa na sababu mbalimbali ikiwemo hali ya uzalendo iliyokuwa ikifanywa
na jeshi hilo ya kuruhusu wananchi kufanya shughuli zao katika maeneo ya jeshi ambapo
baadae wananchi wamehamia katika maeneo hayo.
“Nafahamu katika kambi ya
Itaka kuna mgogoro wa ardhi na tayari Serikali
imetambua maeneo yote yenye migogoro ya
ardhi na tumejipanga kwa ajili ya kuitatua. Tayari tumeanzisha kitengo maalumu cha Miliki
ili kiweze kutatua maeneo yote yenye mgogoro ya ardhi nchini”, alisema Waziri
Kwandikwa.
Aliongeza kuwa zoezi hilo
litafanyika kwa kufuata utaratibu ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka na
wananchi wanapata haki zao na jeshi
linaendelea na shughuli zake kama kawaida.
Waziri Kwandika alisisitiza, “Zaidi ya asilimia 50 ya migogoro ya ardhi iliyopo kati ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini na Jeshi la Kujenga Taifa imetatuliwa na maeneo mengi ambayo yalihitaji fidia wananchi wameshalipwa fedha zao, na hii inaonesha kuwa tunao mwendelezo mzuri wa kuendelea kulipa na hivyo tunatafuta fedha ili tuweze kulipa maeneo mengine yanayohitaji fidia.”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...