Afisa Sheria wa Taasisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) Bw.
Zephania Lyamuya akizungumza katika kikao cha kusuluhisha mgogoro wa
kurudiwa wimbo uitwao “Mungu Baba” wa Bi. Upendo Nkone uliorudiwa na
Studio ya Dom -Tune bila ridhaa ya msanii huyo katika kikao kilichofanyika
katika Ofisi za Taasisi hiyo leo Jijini Dodoma.Kulia kwakwe ni msanii wa
muziki wa Injili Bi. Upendo Nkone.
Mlezi wa Dom-Tune studio Askofu Damasi Silivesta(wa kwanza kulia)
wa Kanisa la THE WORLD MINISTRY akifafanua jambo wakati wa kikao cha
kusuluhisha mgogoro wa kurudiwa wimbo uitwao “Mungu Baba” wa Bi.
Upendo Nkone uliorudiwa na Studio hiyo bila ridhaa ya msanii huyo katika
kikao kilichofanyika katika Ofisi za Taasisi hiyo leo Jijini Dodoma,Kulia kwake
ni watayarishaji wa muziki wa Studio hiyo Bw. Kassim Ali na Samweli Yona.
 

 

Na Shamimu Nyaki - WHUSM, Dodoma
TAASISI ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) kimetoa agizo kwa wadau wa kazi za Sanaa kuacha kurudia kazi za msanii bila ridhaa au makubaliano na mmiliki wa kazi hiyo.
 
Wito huo umetolewa leo Feburari 11, 2021 Jijini Dodoma na Afisa Sheria wa Taasisi hiyo Bw. Zephania Lyamuya alipomaliza kusuluhisha mgogoro wa kurudiwa wimbo uitwao “Mungu Baba” wa Bi. Upendo Nkone  uliorudiwa na Studio ya Dom -Tune bila ridhaa ya msanii huyo.
 
Akizungumza katika kikao hicho Afisa Sheria huyo amesema kazi yoyote ambayo imesajiliwa katika Taasisi hiyo tayari ina Hakimiliki hivyo sio ruhusa kwa mtu yeyote kuitumuia bila makubaliano na mmiliki.
 
“Natoa wito kwa Wadau wa Sanaa kusajili kazi zao COSOTA ili watambulike na kulindwa kisheria, pia waje kupata elimu ya haki za kazi zao ili kuepuka migogoro isiyokua na ulazima” alisema Bw. Lyamuya.
 
Kwa upande wake, Msanii Upendo Nkone ameishukuru COSOTA kwa kumsaidia kupata haki katika kazi yake ambayo ilirudiwa bila raidhaa yake huku akitoa wito kwa jamii  kuacha kurudia kazi zake bila ridhaa yake kwakua kazi zake zinalindwa kisheria kwakuwa amezisajili, na kwamba amewaasa wasanii kujisajili BASATA na kusajili kazi zao COSOTA kwa sababu vyombo hivyo vinawatetea wasanii.
 
Vile vile Muandaaji katika Studio ya DOM –TUNE Bw. Kassim Ally amekiri kufanya makosa hayo na kwamba ameahidi kuheshimu maridhiano yaliyofikiwa huku huku akiishukuru COSOTA kwa kumueleza utaratibu unaopaswa kufuatwa iwapo atahitaji kurudia kazi za msanii yeyote.
 
Kikao hicho kimemalizika kwa maamuzi kwamba Studio ya DOM- TUNE ifute wimbo wa msanii huyo  katika mitandao ya kijamii  na kulipa fidia ya kiasi cha fedha walichokubaliana ndani ya mwezi mmoja kuanzia leo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...