Na Leandra Gabriel, Dar es Salaam
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema mama mzazi wa Hayati Rais Dkt.John Joseph Magufuli bado ni mgonjwa na yupo kitandani kwa miaka miwili sasa na Serikali itahakikisha madaktari wanamtibu hadi atakaporejea katika hali yake ya kawaida.
Akizungumza leo Wilayani Chato mkoani Geita wakati wa Ibada ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati JPM, Majaliwa amesema hadi sasa mama mzazi wa Hayati Rais Magufuli yupo kitandani akiendelea na matibabu.
"Nimeongea na Mh. Rais kuhusiana na jambo hili na tutahakikisha madaktari wanamtibu bibi yetu hadi pale atakaporejea katika hali yake ya kawaida." Amesema Majaliwa.
Waziri Majaliwa msiba huo umewagusa watanzania wengi na kama Taifa hawana budi kumshukuru Mungu na kumuenzi Hayati JPM kwa vitendo.
Pia amewashukuru wasanii, waandishi wa habari na watanzania kwa ushirikiano wanaoonesha katika kipindi chote cha maombolezo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...