Na Leandra Gabriel, Dar es Salaam

MKUU wa Majeshi Tanzania CDF Venance Mabeyo amesema hadi sasa  nchi na mipaka yake  ni salama na wataendelea kumlinda  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan na kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

CDF Mabeyo ameyasema hayo leo Machi 26 wakati wa ibada ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Joseph Magufuli Wilayani Chato mkoani Geita ambapo amesema kuwa kwa niaba ya wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini anahakikisha uimara wa ulinzi na usalama ambao pia utaendelea kuimarishwa.

"Tutaendelea kukulinda ukiwa Rais wa Tanzania na Amiri jeshi mkuu na sio Amirati kama ilivyokuwa inapendekezwa, vyombo vya ulinzi na usalama vitaendelea kukutii na kutekeleza majukumu yetu kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.'' Amesema CDF Mabeyo.

Aidha Mabeyo amesema vyombo vya ulinzi vinamhakikishia Rais Samia  uadilifu, utii na uaminifu kwa mujibu wa mila na desturi za majeshi katika kuhakikisha ulinzi na usalama kama ilivyokuwa katika awamu zote za uongozi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...