Balozi wa Morroco nchini Tanzania Abdelilah Benryane(wa kwanza  kulia) akizungumzia siku ya kimataifa ya kusherehekea lugha ya Kifaransa duniani ambapo ametumia nafasi hiyo kuelezea uzuri wa lugha hiyo na jinsi inavyoendelea kuzungumzwa na mamilioni ya watu duniani kote.

Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederick Clavier(wa pili kushoto) akizungumza kuhusu siku ya kimataifa ya kusherehekea lugha ya Kifaransa ambapo ameelezea jitihada zinazoendelea katika kuhakikisha Watanzania wengi nao wanazungumza lugha ya Kifaransa.

Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederick Clavier(wa tatu kushoto) akifafanua jambo kuhusu umuhimu wa kuzungumwa kwa lugha ya Kifaransa duniani.Wengine katika picha hiyo ni mabalozi wa nchi mbalimbali wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania ambao nao wanazungumza Kifaransa.
Balozi wa Canada nchini Tanzania Pemela O'Donnell (wa kwanza kulia) akizungumza mbele ya waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu siku ya kushererekea lugha ya Kifaransa duniani.
Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania Peter Van Acker akizungumza wakati wa mkutano uliondaliwa a Ubalozi wa Ufaransa nchini kwa kuwashirikisha mabalozi  ambao nchi zao zinazungumza lugha ya Kifaransa.

wa Ufaransa nchini Tanzania Frederick Clavier(wa pili kushoto) akisisitiza jambo.

Balozi wa Canada nchini Tanzania Pemela O'Donnell (wa kwanza kulia) akifafanua jambo kuhusu siku ya kimataifa ya kusherehekea lugha ya Kifaransa duniani.
Mabalozi wa nchi mbalimbali wakiwa wakiongozwa na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania wakimsikiliza kwa makini Balozi Ubelgiji nchini Tanzania Peter Van Acker alipoamua kuzungumza hotuba yake kwa lugha ya Kiswahili wakati anazungumzia siku ya kimataifa ya kusherehekea lugha ya Kifaransa ambapo amesisitiza umuhimu wa kujua lugha tofauti tofauti.



Na Said Mwishehe, Michuzi TV

UBALOZI wa Ufaransa nchini Tanzania umesema upo kwenye mchakato wa kuandaa programu maalum ya muda mrefu ya kuwa inatoa mafunzo ya lugha ya Kifaransa kwa walimu kati ya 50 hadi 100 kila mwaka ambao wakishaifahamu vema nao watafundisha wanafunzi katika shule zao.

Lengo la kuandaa programu hiyo ambayo kwa sasa bado mazungumzo yanaendelea kati ya Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederick Clavier na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Paramagamba Kabudi pamoja na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Profesa Joyce Ndalichako ili kuona namna nzuri ya kuifanikisha programu hiyo.

Akizungumza leo Machi 10, 2021 jijini Dar es Salaam wakati akielezea siku ya kimataifa ya kusherehekea lugha ya Kifaransa Duniani kote, Balozi Clavier ametumia nafasi hiyo kuelezea mikakati ambayo wanaifanya kuhakikisha lugha hiyo inapata nafasi ya kuzungumzwa na watu wengi nchini Tanzania.

"Tunaendelea na mazungumza na Waziri Kabudi, pamoja na Wizara ya Elimu chini ya Profesa Joyce Ndalichako ili kuwepo na utaratibu wa kufundisha lugha ya Kifaransa kwa walimu wa kada mbalimbali na watakapomaliza nao watakwenda kufundisha wanafunzi.

"Katika programu hiyo iwapo itaanza basi kwa mwaka tutakuwa tunafundisha lugha ya Kifaransa kati ya walimu 50 hadi 100 na hivyo baada ya miaka mitatu au mitano tutakuwa na walimu wengi ambao wanajua kuzungumza Kifaransa.Programu hiyo itakuwa ya muda mrefu wastani wa kuanzia miaka 10,"amesema Balozi Clavier.

Amefafanua kuwa mazungumzo yatakapokamilika watatoa taarifa rasmi ya lini sasa programu hiyo itaanza ingawa kuna Watanzania mbalimbali ambao wamekuwa wakijifunza na kuzungumza Kifaransa.

Aidha amesema wengine ambao watanufaika na programu hiyo itakapoanza ni wanadiplomasia ambao wengi wao wamekuwa wakizungumza lugha zaidi ya moja, na watamani Kifaransa kinakuwa moja ya lugha ambayo itasomwa na kada hiyo.

Kuhusu siku ya kimataifa duniani ya kusherehekea lugha ya Kifaransa, Balozi Clavier amesema kila ifikapo Machi ya kila mwaka familia ya nchi ambazo watu wake wanatumia lugha ya Kifaransa nchini wamekuwa wakikutana na kusherehekea kwa kufanyika matukio mbalimbali.

Amesisitiza kuwa lugha ya Kifaransa imekuwa miongoni mwa lugha ambayo inazungumzwa na mamilioni ya watu duniani kote, na kwamba nchi ya Ufaransa itaendelea na jitihada za kuhakikisha watu wengi zaidi wanazungumza lugha hiyo.

Balozi Clavier ametumia nafasi hiyo kutaja nchi kadhaa ambazo zinazungumza lugha hiyo huku akifafanua kwa Tanzania kumekuwepo na jitihada mbalimbali ambazo zimekuwa chachu kwa Watanzania kujifunza lugha hiyo kupitia programu ambazo zimekuwepo kwa muda mrefu.

Kwa upande wake Balozi wa Ubelgiji  nchini Tanzania Peter Van Acker amesema wamekutana  leo kimaalum kwa ajili ya kusherehekea Francphoinie huku akifafanua nchni Ubelgiji wanazungumza lugha kama Kiholanzi, Kifaransa na Kijerumani."Kuzungumza lugha tofauti ni muhimu sana.

"Leo niko hapa na malozi wenzangu tukiwa na mwenyeji wetu Balozi wa Ufaransa, kwa maana nusu ya watu wangu wanazungumza Kifaransa, kwa bahati mbaya mwaka huu hatutapata fursa ya sawa na mwaka jana ya kukuza lugha nzuri ya Kifaransa kutokana na changamoto ya janga la Corona ambayo imeharibu sherehe zetu.

"Kwa hiyo tutakuwa na sherehe za mkondoni  yaani online , tutakuwa na hafla tatu tofauti kupitia njia ya mtandao , kwanza tutaonesha jinsi ya kuoka waffle ambayo ni keki ndogo  iliyookwa kwa chuma na kukaushwa maarufu nchini Ubelgiji , pili tutashirikishana nawe uzoefu wa wanafunzi wa kitanzania nchini Ubelgiji, tatu tutatoa habari kuhusu fursa za masomo nchini kwao,"amesema Balozi Acker.

Awali Balozi wa Morroco nchini Tanzania Abdelilah Benryane amezunungumza kwa kirefu kuhusu siku ya kimataifa ya kusherehekea lugua ya Kifaransa duniani huku akitumia nafasi hiyo kuelezea namna ambavyo mamilioni ya watu duniani wamekuwa wakifurahia kuzungumza lugha ya Kifarasa. Amesisitiza umoja na mshikamano kwa familia ya Francophonie na wataendelea kuhamasisha nchi nyingi zaidi watu wake kuzungumza lugha hiyo.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...