Jafary  Kachenje Mkaguzi mkuu wa ndani waWwizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki akiongea na waandishi jiji Arusha.

Na Woinde Shizza , Michuzi TV ARUSHA


WAKAGUZI  ndani bara la Afrika wamekutana jijini Arusha kujadili matumizi ya teknolojia katika utendaji kazi itakayowawezesha kuboresha ukaguzi wao kwa kupitia teknolojia.

Akifungua mkutano wa 7 wa wakaguzi wa ndani wa Afrika (AFIIA) Mwenyekiti wa Taasisi ya wakaguzi hao Emmanuel Johanes alisema kuwa lengo la mkutano huo ni kuleta manufaa katika uchumi wa nchi za Afrika.

Johanes alisema kuwa  pia wataweza kujadili matatizo  mbalimbali ya wakaguzi na kujua jinsi ya kusaidia kuchangia maendeleo ya nchi za Afrika pamoja na suala zima la kuboresha uwezo wa wakaguzi na kujifunza kutoka nchi zingine.

“Hapa tutabadilishana uzoefu kila mmoja atajua nchi nyingine wanafanya nini na ni namna gani na sisi tunaweza kuboresha mikakati mbalimbali ya kupiga hatua katika maendeleo ya kiuchumi.”Alisema Johanes

Alifafanua kuwa yapo matatizo  mbalimbali ya kiutandaji,uhaba wa vifaa vya kufanyia kazi pamoja na uhaba  wa bajeti za kuwezesha kazi kufanyika ambapo katika sekta ya umma bado wakaguzi wana shida nyingi kutokana na kutokuwa na bajeti na vifaa pamoja na mafunzo ya kutosha.

Kwa upande wake Jafary Kachenje Mkaguzi mkuu wa ndani wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki alisema kuwa ili kuweza kuepuka matatizo  ambayo hutokea mara kwa mara,mafunzo ambayo wakaguzi wa ndani hupatiwa yanapaswa kutolewa kwa wakurugenzi na kwa kufanya hivyo yatawasaidia kufahamu umuhimu wa wakaguzi wa ndani katika taasisi zao.

Kwa upande wake  mkaguzi Mkuu wa ndani wa benki ya CRDB nchini Burundi Aloyce Leonard amesema wakaguzi wanatakiwa kuwa na uwezo wa kutoa uhakiki katika taasisi kulingana na mabadiliko ya teknolojia yanavyokwenda na kuendana na teknolojia mpya  ambapo mkutano huu wa 7 unafanyika jijini Arusha kwa siku nne na umejumuisha mataifa mbalimbali barani Afrika ikiwemo nchi ya Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...