Bondia wa uzito wa juu wa ngumi za kulipwa nchini, Shaaban Jongo ametamba kumsambaratisha mpinzani wake kutoka Nigeria, Alanrewaju Durodoro katika kuwania ubingwa wa Afrika (ABU) lililopangwa kufanyika Ijumaa kwenye ukumbi wa Next Door Arena.
Mabondia hao watapinana katika pambano la utangulizi la raundi 10 ambapo siku hiyo bondia Hassan Mwakinyo atazichapa na bondia kutoka Angola, Antonio Maiala kuwania ubingwa wa Afrika wa ABU wa uzito wa super welter katika pambano hilo lililoandaliwa na kampuni ya The Jackson Group Sports chii ya Afisa Mtendaji Mkuu Kelvin Twissa.
Jongo alisema kana kuwa amejiandaa vizuri na pambano hilo na kamwe hata mdharau mpinzani wake kufuatia ushindi wake wa mfululizo dhidi ya bondia Alphonce Mchumiatumbo wa Tanzania na Mmarekani, Shawn Miller.
Alisema kuwa rekodi za Durodoro zinaonyesha jinsi gani bondia huyo alivyo na uzoefu mkubwa katika ngumi za kulipwa kwa kushinda mapambano 34 na kupoteza manane. Jongo mpaka sasa ameshinda mapambano manane, kupoteza moja na kutoka sare mara mbili. Alisema kuwa pambano hilo litamfungulia njia yake ya kucheza kwenye mikanda ya ubingwa wa Baraza la Ngumi za Kulipwa Duniani (WBC) na hivyo lazima ashinde.
“Nipo tayari kwa pambano, najua uwezo wa mpinzani wangu na kamwe sitampa nafasi, natarajia upinzani mkali sana,” alisema Jongo. Durodoro aliyewasili jana alisema kuwa amekuja kuendeleza rekodi yake ya ushindi dhidi ya Jongo.
“Nimekuja kwa ajili ya ushindi na siyo kushinda, nimejiandaa vyema na najua nini cha kufanya siku ya pambano,” alisema Durodoro. Mbali ya kuwasili kwa Mnigeria huyo ma mabondia wawili wa Bulgaria Pencho Tsvetkov na mwanadada Joana Nwamerue waliwasili mapema zaidi tayari kwa mapambano hayo.
Tsvetkov atazichapa na Mtanzania Daniel Matefu katika pambano la uzito wa juu wakati Joana atazichapa na Mtanzania Leila Yazidu katika pambano la uzito wa super-light.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Jackson Group Sports, Kelvin Twissa alisema kuwa mabondia wengine Sibusiso Zingange, Antonio Maiala na Chris Thompson watawasili leo wakati bondia wa Congo Brazzavile Ardi Ndembo atawasili kesho. Twissa alisema kuwa tiketi zinauzwa kwa sh50,000 kwa viti za kawaida na Sh200,000 kwa viti maalum. Tiketi hizo zinauzwa kwa njia ya ontapp na Nilipe katika pambano hilo lililodhaminiwa na KCB Bank, Tanzania Tourist Board, DStv, Onomo Hotel, M-Bet na Plus Networks Ltd.

Bondia wa Nigerian Alanrewaju Durodoro (wa pili kushoto) na kocha wake Adefemi Babafemi (wa pili kulia) wakiwasili uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kwa pambano la Ijumaa dhidi ya Shaaban Jongo wa Tanzania katika Rumble in Dar 2 kwenye ukumbi wa Next door Arena. Wengine katika picha ni maofisa wa kampuni ya Jackson Group Sports.
Mabondia hao watapinana katika pambano la utangulizi la raundi 10 ambapo siku hiyo bondia Hassan Mwakinyo atazichapa na bondia kutoka Angola, Antonio Maiala kuwania ubingwa wa Afrika wa ABU wa uzito wa super welter katika pambano hilo lililoandaliwa na kampuni ya The Jackson Group Sports chii ya Afisa Mtendaji Mkuu Kelvin Twissa.
Jongo alisema kana kuwa amejiandaa vizuri na pambano hilo na kamwe hata mdharau mpinzani wake kufuatia ushindi wake wa mfululizo dhidi ya bondia Alphonce Mchumiatumbo wa Tanzania na Mmarekani, Shawn Miller.
Alisema kuwa rekodi za Durodoro zinaonyesha jinsi gani bondia huyo alivyo na uzoefu mkubwa katika ngumi za kulipwa kwa kushinda mapambano 34 na kupoteza manane. Jongo mpaka sasa ameshinda mapambano manane, kupoteza moja na kutoka sare mara mbili. Alisema kuwa pambano hilo litamfungulia njia yake ya kucheza kwenye mikanda ya ubingwa wa Baraza la Ngumi za Kulipwa Duniani (WBC) na hivyo lazima ashinde.
“Nipo tayari kwa pambano, najua uwezo wa mpinzani wangu na kamwe sitampa nafasi, natarajia upinzani mkali sana,” alisema Jongo. Durodoro aliyewasili jana alisema kuwa amekuja kuendeleza rekodi yake ya ushindi dhidi ya Jongo.
“Nimekuja kwa ajili ya ushindi na siyo kushinda, nimejiandaa vyema na najua nini cha kufanya siku ya pambano,” alisema Durodoro. Mbali ya kuwasili kwa Mnigeria huyo ma mabondia wawili wa Bulgaria Pencho Tsvetkov na mwanadada Joana Nwamerue waliwasili mapema zaidi tayari kwa mapambano hayo.
Tsvetkov atazichapa na Mtanzania Daniel Matefu katika pambano la uzito wa juu wakati Joana atazichapa na Mtanzania Leila Yazidu katika pambano la uzito wa super-light.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Jackson Group Sports, Kelvin Twissa alisema kuwa mabondia wengine Sibusiso Zingange, Antonio Maiala na Chris Thompson watawasili leo wakati bondia wa Congo Brazzavile Ardi Ndembo atawasili kesho. Twissa alisema kuwa tiketi zinauzwa kwa sh50,000 kwa viti za kawaida na Sh200,000 kwa viti maalum. Tiketi hizo zinauzwa kwa njia ya ontapp na Nilipe katika pambano hilo lililodhaminiwa na KCB Bank, Tanzania Tourist Board, DStv, Onomo Hotel, M-Bet na Plus Networks Ltd.
Bondia wa Nigerian Alanrewaju Durodoro (wa pili kushoto) na kocha wake Adefemi Babafemi (wa pili kulia) wakiwasili uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kwa pambano la Ijumaa dhidi ya Shaaban Jongo wa Tanzania katika Rumble in Dar 2 kwenye ukumbi wa Next door Arena. Wengine katika picha ni maofisa wa kampuni ya Jackson Group Sports.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...