Mkuu wa Chuo Kikuu cha Aga Khan Tanzania (AKU) Profesa Joe Lugalla  akizungumza na waandishi wa habari Katika mahafali ya 16 ya Chuo hicho yaliyofanyika kwa njia ya mtandao na baadhi katika ukumbi Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha Udaktari cha Aga Khan (AKU,) Tanzania Profesa Hussein Kidanto akizungumza kuhusiana jinsi wanavyoandaa madaktari katika mahafali ya Chuo hicho,jijini Dar es Salaam.
Mhitimu wa fani ya  Uuguzi Somoe Mohamed akizungumza kuhusiana na kwenda kutumika kwa jamii. 


Na Chalila Kibuda,Michuzi TV

CHUO Kikuu cha Aga  Khan Tanzania (AKU) kimesema kuwa wahitimu katika hicho ni wanaweza kufanya kazi popote pale duniani kutokana umahiri wa upikaji wa wataalam.

Wahitimu wa Chuo hicho 118  wamefanya mahafali  kwa njia ya mtandao kwa baadhi kuingia katika ukumbi.

Akizungumza katika mahafali ya 16 ya Chuo Kikuu cha Aga Khan yaliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo hicho Profesa Joe Lugalla  amesema kuwa Chuo hicho tangu kilipoanzishwa  kimekuwa kinatoa katika fani ya elimu,udaktari bingwa pamoja na Uugugzi na ukunga na wanahitimu wamekuwa wakifaya vizuri katika sehemu zao za kazi.

Profesa Lugalla amesema katika udahili wanafanya kwa kuzingatia idadi ya walimu na sio kujaza wanafunzi katika  madarasa.

Amesema kuwa  wahitimu wanachotakiwa kufanya ni kusimamia taaluma zao sehemu za kazi  na kuleta tija katika maendeleo ya nchi.

Kwa upande wa  mkuu wa Chuo cha Udaktari Chuo Kikuu cha Aga Khan Tanzania, Profesa Hussein Kidanto  amesema katika uandaji wanafunzi wa ngazi ya uzamili wanafanya mafunzo  katika Hospitali ya Aga Khan ambayo ina kila kitu.

Profesa Kidanto amesema kuwa wahitimu wameandaliwa na kwenda kuleta mabadiliko katika utoaji wa huduma katika Sekta ya afya.

Mhitimu wa ngazi ya Uuguzi Somoe Mohamed amesema kuwa anakwenda kubadili mtazamo wa wauguzi wa kutojali wagonjwa na kuwa sehemu ya wauguzi wanaojali wagonjwa.

Amesema mgonjwa akiangaliwa vizuri hata kama ana maumivu yanapungua kutokana na huduma ya muuguzi.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...