Na Mwandishi wetu, Manyara
HAKIMU
wa Mahakama ya Mkoa wa Manyara, Simon Kobelo amemuhukumu Mwenyekiti wa
Chama Cha Mapinduzi CCM Tawi la Maisaka Kati Mjini Babati, Bakari
Khatibu Yangu kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka miwili au kulipa
faini ya laki tatu kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa kutoka kwa
mwinjilisti wa Kanisa la KKKT mtaa wa Komoto Daniel Jacob Tango.
Mkuu
wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Manyara,
Holle Joseph Makungu ameyasema hayo mjini Babati wakati akizungumza na
waandishi wa habari.
Makungu
amesema Mwenyekiti huyo wa CCM Yangu ameingia hatiani baada ya kukiri
makosa kinyume na kifungu cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na
rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Amesema alitenda kosa hilo ili amwachie mwinjilisti huyo kiwanja ambacho Mwenyekiti huyo alikuwa akidai ni mali ya CCM.
Amesema
awali, kesi hiyo namba CC 24/2020 ilifikishwa katika mahakama hiyo na
mawakili wa TAKUKURU Martin Makani na Evelyne Onditi, Juni 26 mwaka 2020
ambapo mshtakiwa alikana mashtaka yake.
"Baada
ya kukana makosa yake mawakili wa TAKUKURU waliwasilisha vielelezo na
ushahidi ulioiwezesha Mahakama kumwona mshtakiwa ana kesi ya kujibu
mashtaka baada ya kutakiwa kujitetea aliamua kutoisumbua mahakama kwa
kukiri makosa yake yote ya kuomba na kupokea rushwa kama
alivyoshtakiwa," amesema Makungu.
Amesema
baada ya kukiri makosa yake Mahakama ikatoa ikatoa adhabu kwa mujibu wa
kifungu cha 15 (2) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba
11/2007 ambapo mshtakiwa Yangu aliweza kulipa faini hiyo ya shilingi
laki tatu na hivyo kukwepa kifungo cha miaka miwili kwenda jela.
"Tunatumaini
kuwa hukumu hii itakuwa fundisho kwa viongozi ndani ya chama tawala
hasa wa ngazi ya chini wenye utajiri wa fikra haba wanapopitapita na
kuwaaminisha wananchi kuwa hawawezi kuguswa na TAKUKURU kwa sababu ni
chama kilichowaajiri na kinaongoza Serikali," amesema Makungu.
Ametoa
rai kwa viongozi wa aina hiyo wakumbuke kuwa ibara ya 13 (1) ( 5) ya
katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza usawa mbele ya sheria
kwa watu wote bila kuzingatia utaifa wao, kabila, pahala walipotokea,
maoni yao ya kisiasa, rangi, dini jinsia na hali yao ya kimaisha.
"Kwa
msingi huo kiongozi wa chama tawala au vyama vingine vya upinzani,
sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 inakuhusu
na inaweza kuchukua mkondo wake pale unapovunja sheria hiyo ili mradi
nafasi hiyo iwe ni kutekeleza majukumu yanayohusiana na umma wa
Watanzania kama ilivyofanya kwa Bakari Khatibu Yangu," amesema Makungu.
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Holle Joseph Makungu akizungumza na waandishi wa habari Mjini Babati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...