**********************

Na.Khadija Seif Michuzi Tv  

MSANII wa Taarab Salha Abdallah Kuwasha Moto Burundi. Akizungumza na Michuzi Tv Nadia Khamis ambae ni Mdau Mkubwa wa Muziki wa Taarab amesema Show hiyo inalenga kunyanyua Muziki huo pamoja na kuusukuma hata nchi zingine zifahamu kuwa Tanzania Kuna Muziki wa aina hiyo.

"Kupitia Mimi ningetamani kuona Muziki wa Taarab unafika mbali zaidi kujulikana na kujitangaza ili tuweze kupata nafasi ya kuonyesha upekee tulionao na Sauti za kipekee kutokana nchini kwetu."

Aidha,Nadia ameeleza kuwa katika show hiyo aliyoipa jina la "Pambe za vijora"  Sababu ya Kumchagua Salha Abdallah kama Mtumbuizaji sanjari na Bendi ya Taarab ya  Jasmini.

"Ni Msanii ambae Nina ukaribu nae napenda kazi zake hivyo ni wapenzi wa Bujumbura nchini burundi kusubiri Julai 27 mwaka huu kuona Salha akitumbuiza Mubashara jukwaani.

Pia amesema show hiyo ni moja ya zawadi kwa nchi ya Burundi kutokana na takribani miaka 14 kutokuwepo kwake huko kwani ni  sehemu ya Makazi yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...