Kampuni ya  Gf Trucks & Equipment’s Ltd  ya jijini Dar es Salam imewaomba Watanzania hasa wadau wa sekta ya ujenzi na usafirishaji kupenda kununua bidhaa za ndani ili kusaidia kukuza uchumi.

Akizungumza  katika banda la Kampuni hiyo lililopo Viwanja vya Sabasaba, Afisa Masoko wa GF Truck Juma Lukolo amesema, kama Watanzania watajenga utaratibu wa kununua bidhaa za ndani basi pia wataokoa fedha nyingi za kigeni.

Amesema Watanzania wamekuwa wakitumia fedha nyingi za kigeni na tena kwa gharama kubwa  kuagiza magari kutoka nje, hivyo kwa magari haya kutengenezwa humuhumu nchi kutaokoa muda, gharama na kusaidia kukuza uchumi wa ndani.

"Kwa sasa yale magari tuliyokuwa tukiagiza na kuyauza kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kimaendeleo sasa tunayatengeneza hapahapa nchini kwa lengo la kukuza uchumi, kutoa ajira kwa Watanzania huku tukikuza uchumi.

Kiwanda kinachotengeneza magari hayo cha GF Truck and Car Assemble ambacho kipo ndani ya majengo ya iliyokuwa Tamco.

Afisa Masoko wa GF Truck Juma Lukolo akizugumza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...