Na John Walter-Manyara

Mbunge wa Jimbo la Babati mjini (CCM), ambaye pia ni Naibu waziri wa Sanaa,Utamaduni na Michezo Pauline Gekul, anatarajia kuanzisha  mashindano ya Michezo mbalimbali yenye jina Gekul Cup 2021, yatakayoshirikisha kata zote nane za jimbo hilo kuanzia Oktoba 1 mwaka huu.

Akizungumzia mashindano hayo akiwa ofisi ya Jimbo mjini Babati leo Septemba 22,2021 Gekul alisema lengo la mashindano hayo ni kuibua vipaji, kutoa fursa za ajira kwa vijana pamoja na kuleta mshikamano katika jamii yakiongozwa na kauli mbiu isemayo “Kipaji ni Uchumi”.

 Gekul alisema kwa sasa hakuna sekta inayofanya vizuri katika kutoa ajira kwa vijana kama michezo huku akisistiza umuhimu wa kushiriki michezo kwa lengo la kuhamasisha Amani na kuimarisha afya.

Gekul amesema Mashindano hayo yatakuwa katika michezo ya Mpira wa Miguu kwa wanaume na wanawake,mpira wa pete na Riadha ambapo itafanyika katika ngazi ya kata kwenye kata zote na mitaa yake na washindi watakutanishwa kwenye mchujo na kupata mshindi wa jimbo.

Naye mjumbe wa kamati ya Gekul cup 2021 ambaye pia ni kiongozi wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Babati (BDFA) Mwalimu Dennis Bakuza alisema maandalizi yanaendelea vizuri.

Kuhusu Zawadi zitakazotolewa kwa washindi Bakuza amesema zitatangazwa baadaye.

Kata zitakazoshiriki mashindano hayo ni Maisaka, Bagara,Sigino,Mutuka,Nangara,Singe,Bonga na Babati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...