Lengo la semina hiyo ikiwa ni kuwapa uelewa wabunge na watumishi kuhusu uwekezaji kwenye mifuko ya uwekezaji wa pamoja.
Mkurugenzi
Mtendaji wa UTT, Simon Migangala alisema kuwa Mifuko ya Uwekezaji wa
Pamoja inatoa unafuu wa kuwekeza kwenye hatifungani, akaunti za muda
maalum na hisa za makampuni yanayofanya vizuri ambapo mwekezaji ana
uwezo wa kupata hisa zote ambazo mfuko umewekeza kwa ununuzi mmoja.
Kwa
upande wake Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai, aliupongeza mfuko huo kwa
kuandaa semina hiyo ambayo imetoa fursa kwa wabunge na watumishi kupata
elimu juu ya Uwekezaji Wa Pamoja. "Kuna faida kubwa ambazo mtu anaweza
kupata kwa kuwekeza katika mifuko inayosimamiwa na UTT AMIS". Alisema
Spika Ndugai.
Mifuko
ya uwekezaji wa pamoja inaratibiwa na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na
inadhibitiwa na sheria ya mifuko ya uwekezaji wa pamoja yenye lengo la
kumlinda mwekezaji. Kanuni hizi zinahusiana na shughuli za kampuni za
Usimamizi/Uwendeshaji wa mifuko ya uwekezaji wa pamoja.
Mkurugenzi
Mtendaji wa UTT, Simon Migangala, akitoa elimu ya fursa zinazopatikana
kwenye mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja kwa wabunge na watumishi wakati wa
semina iliyofanyika jijini Dodoma mwishoni mwa wiki.Spika wa Bunge, Job Ndugai akisisitiza juu ya umuhimu wa kuwekeza kwenye mifuko ya uwekezaji ya UTT AMIS.
Spika mstaafu Pius Msekwa akitoa ushuhuda jinsi alivyonufaika na mifuko inayosimamiwa na UTT AMIS.
Mmoja wa wabunge akiuliza swali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...