Na Khadija Kalili

MKUU wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakar Kunenge amezindua Kituo Cha uwezeshaji wa huduma za wawekezaji   kituo cha pamoja (One Stop Center).

 RC Kunenge  alisema kuwa Kitengo hicho kinajumuisha  Watendaji  kutoka  Wizara  na Taasisi  mbalimbali  kwa ajili  ya kurahisisha  mchakato  wa wawekezaji kupata  leseni  za uwekezaji ndani ya Mkoa wa Pwani kwa haraka.

"Lengo ni kuhakikisha wanatoa huduma nzuri kwa wawekezaji Pwani  ili kuwarahisishia  kupata fursa mbalimbali ndani ya Mkoa" alisema Kunenge.

"Jambo hili litaweza kutoa taarifa kwa wadau wa ndani na nje ya Mkoa wetu kwamba una fanya nini na fursa zake zilizomo kuweza kutangazika kwa ujumla alisema.

"Uzinduzi wa Kituo hiki ni agizo la Rais wa awamu ya Sita Mama Samia Suluhu Hassan kama alivyoagiza vituo hivi vianzishwe nchi nzima hivyo na sisi Pwani tumetekeleza" alisema RC Kunenge.

Hivi Sasa tumeshawaandiki EPZA pindi wanapopata mwekezaji lazima taarifa za muhusika  zipite ndani ya kituo hiki.

Awali akizungumza  kabla ya uzinduzi huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani (RAS)  Mhandisi  Hajat Mwanasha Tumbo alisema kuwa sababu zilizopelekea kuanzishwa kwa kituo hiki ni kwa sababu wawekezaji wamekua wakifanya biashara zao bila kujitangaza ipasavyo hivyo baada ya kugundua hilo kuanzia Sasa itabidi wafuate utaratibu wa kufahamika ndani ya Mkoa wa Pwani   kwa sababu awali wawekezaji hai walikua walienda  EPZA  moja kwa moja na baada ya hapo huenda kwenye maeneo ya  uwekezaji bila ya Mkoa kuwatambua, tayari tumewaandikia barua  EPZA  kuwa kuwanzia sasa  wakimpitisha mwekezaji yoyote bila kumpitisha Pwani hatutamtambua hivyo wazingatie utaratibu huu.

Uzinduzi wa kituo hicho umefanyika leo asubuhi, katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani zilizopo Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.

Baadhi ya Taasisi hizo wezeshi  zitakazokuwa zikipatikana ni pamoja na  Idara ya Uhamiaji, Brela, RUWASA, TANESCO, Zimamoto, Utumishi,DAWASCO.TRA, NEMC.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...