Na Humphrey Shao,Michuzi Tv.

RAIS wa Heshima wa klabu ya Simba , Mohamed Dewji 'Mo' ametuma Salam Kwa mashabiki wa Yanga ambao ufika kuizomea Simba katika michezo yake ya kimataifa.

Mohamed Dewji ametoa kauli hiyo Kwa uchungu kwenda kwa baadhi ya mashabiki wa Yanga ambao wameonesha nia ya kwenda Uwanja wa Benjamin Mkapa jumapili hii huku lengo lao likiwa ni kuizomea Simba inapokosea.

"Linapokuja suala la kimataifa, Yanga akicheza na timu yoyote, mimi huwa naiombea dua njema Yanga ifanikiwe kwasababu mafanikio hayatokuwa ya Yanga tu bali ni ya Tanzania kwa ujumla" - @Mohamed Dewji

"Niliumia sana kuona Biashara United imeshindwa kusafiri kwenda Libya kwenye mechi yake ya kimataifa" alisisitiza Mohamed Dewji.

Simba inashuka Dimbani kesho Jumapili kuivaa RS Berkane ya Morocco katika mchezo wa raundi ya pili ya makundi katika kombe la shirikisho barani Afrika.

Simba ndio Timu pekee Kwa ukanda wa Afrika Mashariki (Cecafa) ambayo imebaki katika mashindano makubwa barani Afrika .


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...