JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu: 255-262961500/1 

Nukushi: 255-262961502

Baruapepe: press@ikulu.go.tz

Tovuti : www.ikulu.go.tz               


Dodoma

12 Machi, 2022



Description: Description: Description: Description: Description: Coat of Arms

OFISI YA RAIS,

      IKULU, 

 1 BARABARA YA JULIUS NYERERE,   

CHAMWINO,

S.L.P 1102,

40400 DODOMA.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa agizo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge kuandaa kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.

Rais Samia ametoa maelekezo hayo baada ya kupokea maazimio ya awali kutoka Kikosi kazi alichokiteua cha kufuatilia hoja zilizojitokeza katika mkutano wa wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa uliofanyika jijini Dodoma Desemba 15 hadi 17.

Rais Samia amemwagiza Waziri huyo wa wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge kushirikiana na Tanganyika Law Society (TLS) pamoja na Zanzibar Law Society (ZLS) kutengeneza kanuni hizo.

Kikosi kazi hicho chenye wajumbe 24, na ambacho kinawajibika moja kwa moja kwa Mhe. Rais, kiliwasilisha maazimio hayo Ikulu Jijini Dodoma. Maazimio hayo yamegawanyika katika makundi matatu ya muda wa utekelezaji.

Azimio la muda mfupi ni uandaaji wa kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.

Baadhi ya maazimio ya muda wa kati ni pamoja na Rushwa na maadili katika uchaguzi, Ruzuku, Elimu ya uraia, huku masuala yanayohusu Uchaguzi na Katiba mpya vikiwa ni mpango wa muda mrefu.

Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...