Na Farida Said, Michuzi TV- Morogoro

WAZIRI wa Nishati Januari Makamba amesema Serikali kupitia Wizara hiyo imetumia takribani  Sh.trilioni 3.4 katika kuuendeleza mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere Hydro Power Project na mradi huo utakapokamilika utatoa fursa kwa Watanzania kupata umeme kwa bei nafuu.

Makamba amesema katika katika kipindi cha mwaka moja tangu Rais Samia  Suruhu Hassani kuingia madarakani ameidhinisha na kulipa kiasi cha shilingi Tririoni  1.4  ikilinganishwa na tririoni 2. zilizokuwa zimelipwa awali huku mradi umefikia asilimia 56 kutoka asilimia 40 ya awali.

Akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini iliyotembelea mradi huo, Waziri Makamba amesema Wabunge wa kamati hiyo  wameridhishwa na   kufurahia hatua iliofikia, wamepongeza serikali , Wizara na TANESCO  na  Rais kwa uwezeshaji  wake na idhini yake ya kutoa malipo  kwa wakati.

Ameongeza kasi hiyo ya mradi imetokana  kufanyika kwa mabadiliko ya  uongozi   na uendeshaji  katika mradi huo  ili kuhakikisha ubora na viwango vinafikiwa.Katika mabadiliko hayo yamehusisha mfumo mzima wa usimamizi wa mradi kwa kuongeza wataalam na utaalamu zaidi, sambamba na kumhimiza mkandarasi  naye aongeze wataalamu wengi zaidi wenye uzoefu mkubwa wa miradi kama hiyo .

Hata hivyo amesem walibadilisha mfumo wa mawasiliano kati ya Wizara na TANESCO ,Mkandarasi na TANESCO pamoja na Mhandisi mshauri.’Yapo mambo ambayo tunaendelea kuyafanyia kazi  ambayo yapo ndani ya uwezo wetu,lengo ni kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati, ili kuongeza  kiwango cha umeme nchini  kwa gharama nafuu "

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge  ya Nishati na Madini , Dustan Katandula amesema kamati hiyo imeridhishwa na utekelezaji wa mradi huo kwa sasa ambapo kuna tofauti kubwa na awali walipotembelea mradi huo.‘’ Tuendelee kuiomba Serikali  iendelee kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mredi huo, ili  maratajio ya Watanzania  kuona mradi huu unakamilika kwa wakati "

Wakati huo huo Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO  Maharge Chande amesema zipo changamoto chache zilizofanya maradi huo kuchelewa ikiwemo ya  ugonjwa wa UVIKO 19 ambapo ilisababisha  ucheleweshaji wa baadhi ya vifaa,   kwa sasa wanafanya tathimini   ya muda gani  utakaoongezeka  katika mradi huo.

Ameongeza katika asilimia 56 za mradi ulipofikia hadi sasa, ina sehemu nane na dani yake, ikiwemo njia za kupitishia maji, nyumba za wafanyakazi, tuta kuu, mashine za kuzalishia umeme, kuta za kuzuia maji yasitoke na ujenzi wa daraja katika bwawa hilo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...