Na Khadija Kalili

Uongozi wa Jumuiya ya Wanawake  wenye ulemavu nchini (SHIVYAWATA) wameandaa sherehe Yao ya  maadhimisho ya siku ya wanawake duniani  ikiwa hii  ni siku  maalumu kwa ajili ya wanawake w wenye mahitaji maalumu.

Maadhimisho hayo ya siku ya wanawake  kwa upande wa  wanawake wenye  ulemavu yamepangwa kuadhimishwa Machi 23  katika Ukumbi wa Millennium Tower Dar es Salaam.

Akifafanua lengo  la kuandaa maadhimisho ya  siku hii kwa wanawake wenye ulemavu  Mwenyekiti  wa Jumuiya ya  Wanawake na Watoto (SHIVYAWATA),  Nuru Awadh alisema  ni kuangazia  mwaka  mmoja  wa uongozi wa Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan  anayetimiza mwaka mmoja tangu alipoingia madarakani mwezi Machi mwaka jana.

"Lengo la kuanzisha siku hii muhimu kwa wanawake wenye ulemavu  ni kuangazia mwaka  mmoja  wa uongozi wa Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan, pamoja na kuelezea juhudi alizozifanya katika  kutekeleza  haki za wanawake  na watoto hasa wenye ulemavu Ili kukuza  uchumi wa haki  na usawa  kwa  maendeleo endelevu, Jumuiya ya Wanawake wenye ulemavu tunasema  sambamba na kuangazia  juhudi  alizozifanya  katika  kutekeleza haki za  wanawake  na watoto hasa wenye ulemavu Ili kukuza uchumi wa haki na usawa kwa maendeleo endelevu"alisema Mwenyekiti huyo.

Kwa upande wake Mweka hazina wa Jumuiya hiyo Christina Silas alisema wanawake wenye ulemavu wanasema kuwa wanamshuku sana Mheshimiwa Rais Samia kutokana na  kuanzishwa kwa Wizara  ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wanawake na Makundi Maalum.

"Mheshimiwa Rais Samia ametoa  maelekezo kwa Wizara  kuchukua  hatua  kutatua  changamoto za watu wenye  ulemavu, kuteuliwa  kwa watu wenye  ulemavu kwenye nafasi za maamuzi,pia tunashkuru  kuona kwamba zoezi la Sensa ya Taifa kuzingatia umuhimu  wa kukusanya taarifa  za watu  wenye ulemavu, kuendelea kutolewa  asilimia kumi  za Halmashauri kwa ajili ya  Wanawake , vijana  na wenye ulemavu na kuendelea kufanya maboresho"alisema Christina.

Christina aliongeza kwa kusema kuwa pamoja na  mafanikio waliyoyafikia zipo changamoto nyingi  wanakabiliana nazo wanawake wenye ulemavu huku akisema kuwa Machi 16 mwaka huu Mheshimiwa Rais Samia atakapokutana na viongozi  wa vyama vya watu wenye ulemavu katika Mkutano utakaofanyika Ikulu  Dodoma Mjini  basi aweze  kutilia mkazo na kutoa suluhisho  katika changamoto wanazokabiliana nazo ambazo ni  ajira kwa  wanawake wenye ulemavu bado ni tatizo.

Silas alisema  kuwa  wanawake wenye ulemavu wamekuwa wakikumbana na changamoto nyingi pindi wanapokwenda  kwenye vituo  na hospitali Ili kupata  huduma za afya  hasa vyumba vya kujifungulia watoto, vitanda vya kujifungulia   kutokuwa na mazingira rafiki   kwa walemavu kwani huwa ni virefu sana hivyo tunaomba kwenye hospitali zetu kuwe  na vitanda maalumu kwa ajili ya kujifungua walemavu  kwa ujumla tunaomba pindi mlemavu anapokwenda kujifungua  aruhusiwe  kuwa na wasaidizi wake hata wakalimani wa lugha tofauti na ilivyo sasa.

Siku ya wanawake duniani huadhimishwa kila ifikapo Machi 8  Kila mwaka.

Kutoka kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wenye ulemavu (SHIVYAWATA) Nasria Nasir (ambaye ni mlemavu wa kuzungumza)  akifuatiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Nuru Awadh ambaye nimlemavu wa macho akifuatiwa na Mweka Hazina Christina Silas na Katibu wa Jumuiya hiyo Maria Chale  (Wote wakiwa ni walemavu wa ngozi Albino).







  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...