Na Karama Kenyunko, Michuzi TV

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) imetakiwa kufanya mapitio ya sheria na sera zilizopo ili kuhakikisha bunifu zinazozalishwa zinatatua changamoto zilizopo  katika jamii.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Juma Kipanga wakati alipotembelea banda la Costech katika maonesho ya 46 ya Sabasaba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.

Amesema wakati sheria hiyo inaanzishwa kulikuwa hakuna eneo la ubunifu ndani yake ndiyo maana wanataka kufanya mapitio hayo, kwa sababu wanataka bidhaa zinazobuniwa ziweze kutatua changamoto hapa nchini.


Amesema wamepiga hatua kama taifa kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali kupitia bunifu za ndani  hivyo ni lazima kuhakikisha bunifu hizo zinawanufaisha kwa kutengeneza ajira.

Hata hivyo, Kipanga amesema wameona wabunifu mbalimbali walivyoendelezwa na Costech, kabla ya hapo walikuwa na mfuko wao na pia kuna mashindano yanaitwa makisatu.


"Vyombo vyote hivi vimeundwa kuhakikisha kwamba bunifu pamoja na tafiti zinaweza kukuzwa na kuendelezwa ili badae ziwe bidhaa," amesema Kipanga.


Kipanga ametoa rai kwa Costech kuendelea kufanya kazi na kushirikiana kwa sababu Taifa hili litajengwa na watanzania wenyewe na lengo la bunifu hizi ni kuhakikisha zinatatua changamoto.


"Tutatumia bunifu zetu za ndani kwa sababu ni rahisi kupata bidhaa inayoweza kutatua changamoto kwa bei rahisi na pia inaweza kutumika kwa urahisi,"amesema  Kipanga







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...