MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Fatma Abubakar Mwasa leo  20 Agosti, 2022, ametembelea banda la TAWA katika viwanja vya Gymkhana Mkoani Morogoro ambako Mbio za riadha za  'Selous Marathon' zimefanyika.

Akiwa katika banda la TAWA, Mhe. Mwasa aliweza kupata maelezo mafupi kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na TAWA.

TAWA imetumia mbio riadha za 'Selous Marathon' kutangaza vivutio vya utalii  vinavyopatikana katika  Pori la Akiba la Selous lililopo mikoa ya Lindi na Pwani, Pori la Akiba Pande lililopo jijini Dar es Salaam na Pori la Akiba Wamimbiki lililopo Mkoani Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...