Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla akiangalia mifuko ya Plastiki ambayo haitakiwi kutumika hapa nchini ili kulinda mazingira.

*Wazalishaji Mifuko mbadala waomba Serikali kuchukuwa hatua.
* NEMC na TBS Watoa tamko la kusimamia Operesheni, Wataka Mikoa ya mipakani kuimarisha Udhibiti.
* RC aagiza kuhitishwa kikao Cha Wenyeviti wa Masoko DSM.

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla leo August 19 ametangaza Operesheni ya kukamata Mifuko ya plastic iliyokatazwa na kuwataka Wananchi kujiepusha na Matumizi ya Mifuko hiyo.

RC Makalla ametangaza Operesheni hiyo wakati wa kikao kazi Wazalishaji Mifuko mbadala, Kamati ya Ulinzi na usalama na Mamlaka za Udhibiti ikiwemo TBS na NEMC Baada ya kubaini Mifuko iliyokatazwa imeanza kurudi upya.

Aidha RC Makalla ameagiza kuhitishwa kikao Cha Wenyeviti wa Masoko yote ya Mkoa huo na kutolewa maelekezo ya katazo la uuzaji wa Mifuko iliyokatazwa kwenye Masoko yao.

Pamoja na hayo RC Makalla ameelekeza Mamlaka ya Udhibiti na usimamizi wa Mazingira NEMC kurudi upya kutoa Elimu kwa Wananchi kuhusu Madhara ya Matumizi ya Mifuko hiyo.

Miongoni mwa Madhara ya Matumizi ya Mifuko iliyokatazwa ni Uchafuzi wa Mazingira, Ukwepaji wa Kodi Kutokana na Mifuko Kuuzwa kinyemela pamoja na kuua viwanda vilivyopewa kazi ya kuzalisha Mifuko mbadala.

Kwa upande wao Mamlaka za Udhibiti kupitia Wakurugenzi wa NEMC na TBS wametumia kikao hicho kutoa tamko la kusimamia Operesheni hiyo ambapo wamemuahidi RC Makalla kuwa Operesheni hiyo itafanikiwa.

Wazalishaji wa Mifuko mbadala wamekiri uzalishaji wa Mifuko iliyoruhusiwa kudorora Kutokana na kuzagaa kwa Mifuko iliyokatazwa kwenye Masoko na Maduka jambo linalopelekea viwanda vyao kufa ambapo wameiomba Serikali kusimamia Operesheni hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...