Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Taasisi ya Wanawake Jikoni Bussiness na mwandaaji wa tamasha hilo Nice Mamuya (katikati,) akizungumza na waandshi wa habari kuelekea kilele cha tamasha la Mama Ntilie 2022 litakalofanyika tarehe 2 na kuhitimishwa tarehe 3 Septemba mwaka huu katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa tamasha hilo la  la Mama Ntilie limedhamiria kulitangaza kundi hilo na kuwa kundi rasmi kama makundi mengine yanayojihusisha na shughuli za ujasiriamali kushoto ni Lenin Rugaimukamu mtafti wa masoko kutoka Bwana Sukari na kulia ni  Mkurugenzi kutoka taasisi ya Wanawake Jikoni Bussiness Sheree Andersen.

 

TAMASHA kubwa la kumtafuta Mama Ntilie bora kwa mwaka 2022 linatarajiwa kufanyika Septemba mbili na tatu mwaka huu katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam kwa mchuano mkali wa Mama Ntilie watano kutoka katika Wilaya zote za jijini la Dar es Salaam huku Waziri wa  Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima  akitarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha tamasha hilo likitalofanyika Septemba 3.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijinii Dar es Salaam mwanzilishi na Mkurugenzi wa  Taasisi ya Wanawake Jikoni Bussiness na mwandaaji wa tamasha hilo Nice Mamuya amesema kuelekea kilele cha tamasha la Mama Ntilie litakalofanyika tarehe 3 katika viwanja vya Leaders jijini humo litakwenda sambamba na malengo ya taasisi hiyo kwa kuchochea fikra za wanawake, kuamsha hali chanya ya maendeleo kwa wanawake pamoja kuwajengea uwezo, maarifa, teknolojia na mitaji.

Amesema tamasha hilo la  la Mama Ntilie limedhamiria kulitangaza kundi hilo na kuwa kundi rasmi kama makundi mengine yanayojihusisha na shughuli za ujasiriamali na  litahudhuriwa na vongozi wa Serikali, taasisi binafsi, wadau wa maendeleo na wajasiriamali.


'' Kwa kushirikiana na Clouds Media tumeandaa tamasha hili pia kwa kuhakikisha kundi hili linakuwa zaidi...Wananchi tujitokeze katika siku ya kilele tarehe tatu kuanzia saa saba mchana na kushuhudia mambo makubwa yanayofanywa na kundi hili muhimu katika maeneo yote nchini'' Amesema.

Amesema, wameanza tamasha hilo jijini Dar es Salaam na wataliendeleza katika mikoa mingine ya Tanzania na kuwataka akina Mama Ntilie kujiandaa kulipokea tamasha hilo katika mikoa yao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa taasisi ya Wanawake Jikoni Bussiness Sheree Andersen amesema, kuelekea kilele cha tamasha hilo Mama Ntilie watafanya mashindano siku ya tarehe mbili kwa kuwahusisha Mama Ntilie 5 kutoka katika Wilaya zote za jiji la Dar es Salaam na mshindi atapatikana kupitia mtihani na vitendo vya kazi na atatangazwa siku ya kilele na kukabidhiwa zawadi kubwa ambazo zimetolewa na wadhamini.

Amesema vigezo vilivyotumika kupata washiriki ni pamoja Mama Ntilie mtanzania, mwenye umri wa miaka 18-35, usafi katika biashara, bei ya chakula, idadi ya wateja anaowahudumia, sehemu anaponunua bidhaa pamoja na ubora wa huduma anayoitoa kwa wateja.

Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya Kilombero Sugar Company Limited kupitia bidhaa ya Bwana Sukari mtafti wa masoko kutoka kampuni hiyo Lenin Rugaimukamu amesema kampuni hiyo inatambua mchango wa akina Mama wajasriamali  na udhamini wao umelenga kushirikiana na kundi hilo la wajasiriamali muhimu na watatoa bidhaa yao ya sukari ikiwa ni kiungo muhimu katika shughuli zao za mapishi.

Pia Maimuna Hassan ambaye ni Meneja Masoko wa Nice & Free Pads amesema kampuni hiyo imedhamini kutokana na mchango mkubwa wa akina Mama Ntilie katika kujenga uchumi na ndio watumiaji wakubwa wa bidhaa ya kampuni hiyo na watatoa bidhaa hiyo ya Nice & Free Pads  ili kuwaweka huru na salama Mama Ntilie wakati wakitekeleza majukumu yao.

Pia Evelyn Marriot kutoka Bongo Toothpick amesema wamedhamini tamasha hilo la Mama Ntilie kutokana na umuhimu wa kundi katika jamii  pamoja na ushirikiano wanaoupata kutoka kundi hilo ambalo ni wateja wakubwa wa bidhaa zao ambazo zinatengenezwa nyumbani.

Tamasha hilo la Mama Ntilie 2022 linalokwenda na kauli mbiu ya 'Msosi Uendelee...' limedhaminiwa na Clouds Media, Red Cross, Bwana Sukari, Bongo Toothpick, Nice & Free Pads,Pepsi, Afta water, Cello na Assemble Insuarance.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...