
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali kama ifuatavyo:
1) Amemteua Dkt. Boniphace Christopher Luhende kuwa Wakili Mkuu wa Serikali. Kabla ya uteuzi huu Dkt. Luhende alikuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali. Dkt. Luhende anachukua nafasi ya Bwana Gabriel Paschal Malata ambaye aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.
2) Amemteua Bi. Sarah Duncan Mwaipopo kuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali. Kabla ya uteuzi huu Bi. Mwaipopo alikuwa Wakili wa Serikali Mkuu katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bi. Mwaipopo anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Luhende ambaye ametuliwa kuwa Wakili Mkuu wa Serikali.
Uteuzi huu umeanza tarehe 09 Oktoba, 2022.
Zuhura Yunus
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...