Na Farida Mangube Morogoro.

Mwenyekiti wa kamati ya wanawake Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Rehema Ludanga amesema swala la ukatili wa kijinsia na unyanyasaji mahala pakazi umezidi kushamiri,na kwamba katika maeneo mengi wafanyakazi hasa wanawake hawapewi fursa ya kuonesha uwezo wao

Akizungumza na waandishi wa habari mkoni Morogoro Rehema amesema katika kuadhimisha ya siku ya wafanyakazi Duniani ni vyema serikali ikaandalia kwa kwa umakini maswala ya ukatili wa kijinsia, kwani changamoto hiyo ni kubwa na huwakuta hadi viongozi walio kwenye ngazi mbalimbali.

“ Nitumie fursa hii tunavyo adhimisha siku ya wafanyakazi Duniani kuwaomba viongozi hasa wanaume waache unyanyasaji wa kijinsia, kama kuna kiongozi mwanamke apewe fursa kulingana nafasi yake, kama kunamfanya kazi mwanamke apewe nafasi yake bila ya kujali jinsi” alisema Ludanga.

"Viongozi mara nyingi wanaona aibu kusema kama wananyanyaswa ama kufanyiwa ukatili kwa sababu ya kuangalia mtazamo wake katika jamii unamuonaje, wale watu wa chini wanamuheshimu hawajui kile anachokifanyiwa kwahiyo anaona aibu kutangaza hivyo kuendelea kuumia ndani kwa ndani bila kusema na kitendo cha kukaa kimya kinaruhusu ule ukatili na unyanyasaji unaendele kukua kila siku hadi siku." Alisema

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo wa TUCTA amesema hapa nchini kila mwaka vijana wanao hitimu elimu ya juu ni wengi zaidi ya wanaobahatika kupata ajira rasmi, suala ambalo huenda ni moja ya sababu ya ongezeko la vijana wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

“Ukosefu wa ajira linaweza pia likawa ni chanzo ambacho kinapelekea vijana wetu kurubunika na kudanganyika kuingia kwenye masuala hayo ya ndoa za jisia moja. Alisema

Aidha ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozw na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza asilimia kubwa ya maombi ya wafanyakazi yaliyo wasilishwa kwenye maadhimisho ya mwaka uliopita 2022 ikiwemo kuboresha maslahi ya wafanyakazi, kulipa malimbikizo ya madeni na stahiki kwa wafanyakazi pia kutoa vibali vya ajira mpya.

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Dunia ( Meimosi) kwa mwaka 2023 yamepangwa kufanyika kitaifa mkoani Morogoro ambapo mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Munngano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...