Na Elias Gamaya, Michuzi TV Shinyanga.

Wakazi Zaidi  ya 30,000 wa kata tatu  zaUlowa, Ubagwe na Ulewe zilizo ndani ya wilaya ya kahama mkoani shinyanga  wamekosa huduma za mawasiliano ya barabara kwa siku kadhaa baada ya mvua kubwa kunyesha na kuharibu  daraja la mto Ubagwe.

Wakazi wa  Ene hilo wanasema wanapata adha kubwa ya  Kuvuka Katika Daraja Hilo ambapo wengine hutozwa Shilingi Elfu 5000 Kwa ajili Ya Kuvushwa.

Diwani wa kata ya Ulowa Gabriela Kimaro ameiomba serikali kuchukua hatua za haraka ili wananchi waweze kuondokana na adha hiyo,huku mbunge wa jimbo la Ushetu, Emmanuel Cherehani akiomba wakala wa barabara Tanzania mkoa wa shinyanga (TANROD) kuchukua hatua za haraka kiokoa wakazi wa kata hizo tatu

Kwa upande wake Mhandisi Hans  Kipamila Kaimu meneja wa TANROAD mkoa wa Shinyanga amesema watafanya tathmini changamoto hiyo na kuiwasilisha sehemu husika ili kufanya marekebisho ya barabara hiyo.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...