Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendinga ameagiza ukamilishwa wa haraka shule ya wasichana mkoani humo inayojengwa katika Kijiji cha Kiongozi Halmashauri ya Mji wa Babati na huku akisisitiza kuongezwa kwa idadi ya mafundi ujenzi ili kuongeza kasi ya ujenzi.
Maagizo hayo yametolewa na Mhe. Sendinga Jan 17, 2024 mara baada ya kufanya ziara kwenye mradi huo wenye thamani ya shilingi Bil. 3 ili kujionea mwenendo wa ujenzi na ukamilishwaji wa shule hiyo itakayochukua wanafunzi wasichana wa kuanzia kidato cha Kwanza hadi cha Sita kutoka Mkoani Manyara na Mikoa Mingine.
Mhe. Sendiga ameiagiza Ofisi ya Divisheni ya Elimu ya Sekondari katika Halmashauri ya Mji Babati kwa kushirikiana na Ofisi ya Katibu Tawala Msaidizi Elimu Mkoa kufuatilia na kukamilisha usajili wa shule mapema pale mradi unapokaribia kukamilika.
Aidha, Mhe. Queen Sendiga ametoa pongezi kwa Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaeo Twange pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mji kwa utekelezaji vizuri wa maelekezo yake na kuridhishwa na kasi ya ujenzi ilivyo sasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...