Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini amewataka Wananchi waliopo kwenye Vikundi kuandaa miradi mikubwa itakayowawezesha kukopa kiwango kikubwa cha fedha za Serikali isiyokuwa na riba.

Akizungumza Februari 21, 2024 katika hafla fupi ya kuvunja kikundi cha Amka Mwanamke kilichopo Kitongoji cha Kyamakerya Kijiji cha Nyabange Kata ya Nyankanga Mhe. Sagini amesema mikopo inayotokana na Serikali hususan Serikali za Mitaa inalenga kuwasaidia Wananchi walio kwenye Vikundi wanaoweza kurejesha.

"Lakini twende mbele hivi Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu vinanufaika na mikopo isiyokuwa na riba na tumekubaliana kukopa laki tano au milioni hiyo ni hela ndogo mno hivyo andaeni mradi ambao mkopo mtakaoomba usipungue milioni tano sisi Viongozi tutawaunga mkono"

Pia Mhe. Sagini amesema kuwa mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe lakini mtaji mkubwa kuliko wote ni umoja ambapo wanyonge wakiungana watainuka Kiuchumi kwani Serikali ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira mazuri ya kisera na kisheria yanayoruhusu vikundi kwa kijamii.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Butiama Ndg. Christopher Siagi, amewataka kina mama kuendelea kukiunga mkono na kukiamini Chama Cha Mapinduzi kwa sababu mambo makubwa yote yanayofanywa na Mbunge ni Utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Awali akisoma taarifa ya Risala kwa Mgeni Rasmi Katibu wa Kikundi cha Amka Mwanamke Bi. Rhoda Laurian, alieleza kuwa walianzisha umoja huo Machi 10, 2023 ili kuondokana na mikopo ya kausha damu inayorejeshwa kila siku.

Aidha Mwenyekiti wa Kikundi cha Amka Mwanamke Bi. Monica Mirumbe alimshuku Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini kwa kuridhia kuwa mgeni rasmi katika sherehe yao ya kuvunja kikundi na kuwachangia shilingi laki 858000/- pamoja na viti 50 mbali na maneno yaliyosambaa na kuwakatisha tamaa kuwa Mbunge hawezi kufika kwenye sherehe ya kitongoji.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...