KATIKA kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ajenda ya kuinua wanawake kiuchumi, Benki ya Mwalimu Commercial imezindua bidhaa mpya ya ‘Tunu’ kwa ajili ya Wanawake na Vijana .

Hayo yamebainishwa jijini Dar es salaam na Mkuu wa Kitengo cha ukuzaji biashara na masoko kutoka Benki hiyo,Leticia Ndongole katika halfa ya kusherekekea siku ya Wanawake duniani iliyowakutanisha Jukwaa la viongozi wanawake wa Mashirika ya umma, taasisi na wanasiasa wakongwe.

“Kwa mwaka 2024 tumeona tuweze kushirikiana na Taasisi za umma sambamba na kumuunga mkono Rais Dkt Samia katika ajenda ya kuinua wanawake”amesema Leticia.

Amesema wamekuwa wakitoa huduma kwa walimu Tanzania nzima pamoja na wanawake waliopo katika ngazi zote katika jamii.

Aidha ameongeza kuwa katika kuazimisha siku ya wanawake Dunia Machi 8 wameona ni vema kushirikina na wanawake p katika kuzindua bidhaa hiyo .

Vilevile amesema wanawake wamekuwa wakisukumwa na ajenda moja ya kumuwezesha ili kuharakisha maendeleo ya kiuchumi Kwa Taifa .

“Tumeona ni vema kuzindua bidhaa hii ya tunu tunaamini Kwa ushiriki wa wakuu wa Taasisi za umma tutaweza kuwafikia wanawake wengi katika ngazi zote “amesema na kuongeza:

“Asilimia kubwa ya wanawake ndio wamekuwa wakikuza uchumi hasa katika sekta binafsi…Kama Mwalimu commercial Bank tumeona tunaowajibu wa kuhakikisha kwamba tunaweza kuwasaidia wakinamama katika nyanja mbalimbali ikiwemo kuwaingiaza katika sekta ya fedha Kwa kuwapatia elimu katika upande wa kuwekeza na hatimaye kukuza biashara yao” amesema Leticia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...