Na Nasra Ismail, Geita
MBUNGE wa jambo la Busanda Tumaini Magesa ameahidi ndanibya mwezi mmoja na nusu kukamilisha ujenzi wa bweni katika shule ya sekondari Lutozo iliyopo katika mamlaka ya mji mdogo wa katoro mkoani Geita.

Ameyasema hayo asubuh ya Leo aliposhiriki katika kuchimba msingi wa bweni hilo ambalo linatakiwa kutumika katika msimu mpya wa masoma ya kidato cha tano mwaka huu.

Shule ya Sekondari Lutozo imekuwa ikifanyq vizuri katika matokeo ya kidato cha nne kwa takribani miaka 5 hivyo kufanya shule hiyo kupata hadhi ya kuwa na masomo ya kidato cha tano na cha sita.

Magesa pia alipata wasaa wa kusikiliza kero za wananchi ambapo kero kubwa ni utiririshwaji wa maji yenye kemikali kutoka kwenye maplanti kwenda kwenye mito ya maji ya matumizi ya binafamu mbapo mbunge Magesa aliahidi kuita wataalam kupata majibu juu ya usalama wa maji na pia kuongea na wamiliki ili waweze kuzuia utiririshwaji huo.

Nae Diwani wa kata ya Katoro Kigongo Benedict Sweya alimshukuru na kumpongeza mbunge huyo kwa kutoa shilingi milioni 5 kutoka kwenye mfuko wa jambo kwa ajili ya kuanza ujenzi wa bweni hilo.

"Mheshimiwa Mbunge tumeshiriki hapa na mimi matajio yangu kwamba mwaka huu tunaenda kupokea watoto wa kidato cha tano nina imani umewapigia wadau na wamekubali kushiriki kwakuwa wana imani kubwa na wewe na imani ndani ya mienzi hiyo ujenzi utakuwa umekamilika" alisema Kigongo.

Aidha alimuomba mbunge kuwasaidia kupata kisima katika shule hiyo kwani imekuwa changamoto kubwa hata ikiwa shule inaelekea kupata wanafunzi wa bweni ambao wanahitaji maji ya mara kwa mara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...