NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Daniel Sillo amelitaka Jeshi la Polisi kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Haki, weledi na uadilifu na kuhakikisha usalama wa raia na mali zao unaendelea kuimarika.

Mhe. Sillo amesema hayo wakati alipofanya ziara Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dodoma na kuzungumza na Makamisha na Maofisa Wakuu Waandamizi wa Jeshi la Polisi ikiwa ni mara ya kwanza kutembelea Jeshi la Polisi tangu alipoteuliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Aprili 4,2024.

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camillus Wambura amesema kuwa, Jeshi la Polisi limeendelea kutekeleza makujukumu yake kwa weledi na uadilifu katika kuhakikisha shughuli za kila siku za Jeshi hilo zinaendelea kufanyika kwa kutoa huduma bora na zenye viwango kwa wananchi.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...