
Na Mwandishi Wetu
MKESHA mkubwa wa kuvuka nusu mwaka Kufanyika Dodoma Juni 5 ndani ya Ukumbi wa Jakaya Conversion Center
Mkesha huo unaenda kwa jina la ACROSS THE YEAR umeandaliwa na Mtumishi wa Mungu Emanuel Shemdoe chini ya huduma ya LOVE OF CHRIST na waombaji wa kila mwezi Jijini Dodoma.
“Huu ni mkesha mkubwa unao hudhuriwa na watu wa dini zote bila kubagua” Alisema mwalimu Shemdoe
Waimbaji mbalimbali watahudumu katika mkesha huo. Waimbaji hao ni pamoja na Waimbaji - KKKT Arusha Road Praise team, Cathedral Worship team, Essence of Worship,Agape Gospel Band, Pamoja na John Lisu, Sax tulivu la Mose Zamangwa.
Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na madhehebu mbalimbali wamealikwa kushiriki katika mkesha huo.
“ Tumeanza mwaka mpya wa Serikali, tutatumia muda huo wa mkesha kuiombea Serikali na viongozi wote bila kumsahau Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan” Alisema Shemdoe
Mkesha huo unakwenda na ujumbe Wa INAWEZEKANA , IT IS POSSIBLE utaanza kuanzia saa 2 usiku mpaka asubuhi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...