RAIS Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la Elimu la Kimataifa (GPE) ameongoza vikao vya bodi ya taasisi hiyo leo Jijini Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu.
Vikao hivyo vimefunguliwa na Mhe. Reem Al Hashimy, Waziri wa Umoja wa Falme za Kiarabu anayeshughulikia Ushirikiano wa Kimataifa. Umoja wa Falme za Kiarabu umekuwa ni mdau muhimu wa GPE kwa miaka kadhaa sasa.
Katika vikao hivyo, pamoja na wajumbe mbalimbali wakiwakilisha nchi, mashirika ya kimataifa, vyama vya kiraia kutoka kote duniani, n.k, vilihudhuriwa pia na Mhe. Prof. Nasser Al Aqeeli, Naibu Waziri wa Elimu wa Ufalme wa Saudi Arabia akiwasilisha nia ya Ufalme wa Saudia kuendelea kushirikiana na GPE katika kutatua changamoto za elimu msingi (chekechea, msingi na sekondari) katika nchi zinazoendelea.
Kulia kwa Mheshimiwa Rais Mstaafu ni Mheshimiwa Prof. Nasser Al Aqeeli, Naibu Waziri wa Elimu wa Ufalme wa Saudi Arabia. Kushoto kwa Mheshimiwa ni Naibu Mwenyekiti wa Bodi ya GPE Christine Hogan na Mheshimiwa Waziri Reem Al Hashimy, Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Umoja wa Falme za Kiarabu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...