MKUU wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Singida kwa kupata hati safi “Clean Sheet” ya kukusanya zaidi ya asilimia 100 ya lengo la makusanyo kwa miezi saba mfululizo kuanzia Julai 2024 hadi Januari, 2025

Amesema, mkoa wa Singida umejipanga kuendeleza mafanikio hayo na kuchangia zaidi katika pato la serikali.

Dendego ameyasema hayo alipokutana na maofisa wa TRA kutoka makao makuu ambao wapo mkoani humo kwa ajili ya kutoa elimu ya kodi kwa wadau mbalimbali pamoja na kuwatembelea wafanyabiashara katika maduka yao “Mlango kwa Mlango” kwa lengo la kuwapa elimu ya kodi, kuwasikiliza na kutatua changamoto za kikodi zinazowakabili.

“Niwapongeze na nafurahi mkoa wa Singida kupata “clean sheet”, niaamini kwa ushirikiano tulionao na TRA tutaendelea kupata mafanikio, kwa kweli tumejipanga kuchangia zaidi pato la serikali kwa maendeleo ya nchi yetu kwa kuwa tunawapa elimu walipakodi na wanalipa bila shuruti” amesema Dendego.

Naye Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi kutoka TRA, CPA Paul Walalaze amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Singida na kuahidi kuendelea kutoa elimu kwa wadau na wafanyabiashara wa makundi mbalimbali ili kuhakikisha kwamba walipakodi wanaelewa wajibu wao wa kulipakodi kwa mujibu wa sheria pamoja na kuwasaidia namna ya kutumia mifumo ya TRA inayorahisisha ulipaji kodi kwa hiari na kwa wakati.

“TRA itaendelea kuwaelimisha walipakodi na kuwafikia wafanyabiashara na wadau mbalimbali na kuhakikisha kuwa mkoa unaendelea kufanya vizuri katika kukusanya, na tutaendelea kuwaelimisha na kuwapa taarifa muhimu walipakodi wetu ili waweze kulipakodi kwa hiari na kwa wakati”, amesema Walalaze.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...