Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama leo Februari 22, 2025 amefanya ziara ya kukagua miundombinu pamoja na huduma zinazotolewa katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni (Mkata) Mkoani Tanga inayotarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho Februari 23, 2025 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Miongoni mwa wodi alizotembelea na kuzikagua Waziri Mhagama ni pamoja na wodi ya wazazi, mama na mtoto, wodi ya watoto wachanga, wodi ya huduma za dharura pamoja na huduma zinazotolewa katika jengo la wagonjwa wa nje (OPD).
Waziri Mhagama ameambatana na timu kutoka Wizara ya Afya akiwemo, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Dkt. Hamad Nyembea pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Bw. Tumainiel Macha.
Home
AFYA
WAZIRI WA AFYA AKAGUA MIUNDOMBINU,HUDUMA ZINAZOTOLEWA HOSPITALI YA HALMASHAURI WILAYA YA YA HANDENI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...