Na Mwandishi Wetu 

MJUMBE wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT)Taifa na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji wa jumuiya hiyo Mariam Ulega amewataka wananchi wa Msanga kujitokeza kupiga kura kwa sababu ni haki msingi kupiga kura.

Mariam ameyasema  hayo wakati  akizungumza na Wananchi wa Kata ya Msanga wilayani Kisarawe mkoani Pwani ambapo amesisitiza ni vema wakahakiki majina yao katika  daftari la mpiga kura pindi uhakiki  awamu ya pili utakapoanza.

"Pia wale wananchi ambao wametimiza miaka 18 mwaka huu tunawahimiza kujiandikisha katika daftari la Kudumu la mpiga kura ili wakati wa uchaguzi mkuu utakapofika wapate haki yao kikatiba kichagua viongozi kwa maslahi ya Taifa letu."
Aidha amesema kuwa maendeleo yamefanyika chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amefanya masuala maendeleo  yanaonekana hivyo anahitaji kuugwa mkono kwa kumpigia kura.

Mariam amesema kuwa  masuala ukatili wa watoto  yamekuwa ni mengi hivyo lazima wazazi  kuwa sehemu ya walinzi watoto hao huku akieleza hivi sasa hata wanaume nao wanapigwa na wake zao na huo nao ni ukatilii, hivyo ametoa rai kwa  wanawake waache kuwapiga waume zao na kuendelea na maisha ya amani.








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...