Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa maeneo ambayo yamepata fedha nyingi kupitia mradi wa kuimarisha ubora wa Elimu ya sekondari nchini SEQUIP ambapo umepokea zaidi ya Bilioni 36.596.

Fedha hizo ambazo zimetolewa na serikali zimetumika kujenga shule mpya 41 za Sekondari ambazo miongoni mwake ni pamoja na Shule 1 ya wasichana, Shule 1 ya kanda ya Wavulana, Shule za kata 36, Shule 1 ya Amali ya Mkoa, na Shule 2 za Amali za kata.

Hayo yamebainishwa na Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Mwl Vicent Kayombo ambapo amesema kuwa fedha hizo pia zimetumika kujenga Madarasa 77, Matundu ya Vyoo 119, Maabara 19, Mabweni 22, na Nyumba za Walimu 22.

Mwl Kayombo amesema kuwa mkoa wa Dodoma umejenga shule mpya ya wasichana Manchali kwa gharama ya Shilingi Bilioni 4.450 sambamba na ujenzi wa shule mpya ya Amali ya mkoa iliyojengwa katika kijiji cha Manchali wilayani Chamwino kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.6

Mwl Kayombo ameishukuru serikali inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi katika mkoa wa Dodoma kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ambazo zitapunguza umbali wa wanafunzi kwenda shuleni ikiwa ni pamoja na kuondokana na vishawishi njiani, na kuongeza muda wa wanafunzi kujisomea.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...