
Mikopo hiyo itokanayo na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri imekabidhiwa na Mkuu wa Wilaya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua akiwa sambamba na Meneja Mwandamizi wa Uwezeshaji wa CRDB Bank Foundation, Baraka Kilayo.
Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji ni kati ya mamlaka 10 za serikali za mitaa zilizochaguliwa na serikali kutoa mikopo jumuishi kwa wajasiriamali kwa kuzishirikisha taasisi za fedha.
Baada ya kutolewa kwa hundi hiyo, kunaifanya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kufikisha kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 600 ilizozitoa kwa vikundi vya wanawake, vijana na makundi maalumu ambao ndio wanufaika wakuu wa mikopo hiyo.
Mkuu wa wilaya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua akizungumza na vikundi vya Wanawake, vijana na walemavu waliopokea mikopo inayotolewa na Halmashauri ya manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia Benki ya CRDB chini ya Program yake bunifu ya imbeju.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...