Meza kuu wakati wa semina ya utoaji elimu ya sheria ya bima kwa mahakimu wakazi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wa Mkoa wa Dar es Salaam. Semina hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo Septemba 12, 2025.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Awamu Mbagwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya utoaji elimu ya sheria ya bima kwa mahakimu wakazi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wa Mkoa wa Dar es Salaam. Semina hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo Septemba 12, 2025.
Kamishna wa Bima Tanzania (TIRA), Dkt. Baghayo Saqware akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya utoaji elimu ya sheria ya bima kwa mahakimu wakazi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wa Mkoa wa Dar es Salaam. Semina hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo Septemba 12, 2025.

Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
KAIMU Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Awamu Mbagwa, ametoa wito kwa watumishi wa Mahakama kutumia ipasavyo fursa ya elimu ya bima ili kuongeza uelewa utakaosaidia katika utoaji wa haki kwa wananchi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Septemba 12, 2025 wakati wa semina ya utoaji elimu ya sheria ya bima kwa mahakimu wakazi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wa Mkoa wa Dar es Salaam, Jaji Mbagwa amesema elimu ya bima ni nyenzo muhimu katika kukabiliana na changamoto za mashauri yanayohusiana na bima, hususan migogoro ya fidia baada ya ajali, majanga au hasara za kibiashara.

“Napenda kutoa wito kwa watumishi wote wa Mahakama kutumia fursa hii kujifunza kwa makini, kuuliza maswali na kushiriki kikamilifu katika mijadala. Elimu hii itatufaa sisi binafsi, familia zetu na taasisi tunazozihudumia,” alisema Jaji Mbagwa.

Aidha, ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) kwa kushirikiana na Mahakama katika kuwapatia mafunzo hayo, akibainisha kuwa hatua hiyo itaongeza weledi wa Majaji na Mahakimu katika kushughulikia mashauri ya bima kwa haki na kwa mujibu wa sheria.

Jaji Mbagwa alihitimisha hotuba yake kwa kupongeza wadau mbalimbali wa Mahakama walioshiriki katika semina hiyo na kusisitiza kuwa elimu ya bima ni msingi wa uaminifu, uwajibikaji na ufanisi katika utoaji wa haki kwa wananchi.

Kwa upande wake, Kamishna wa Bima Tanzania (TIRA), Dkt. Baghayo Saqware amesema kuwa mamlaka hiyo itaendelea kushirikiana na Mahakama ili kuhakikisha migogoro ya bima inatatuliwa kwa haki na haraka, jambo litakaloimarisha imani ya wananchi kwa sekta hiyo.

“TIRA imejipanga kutoa elimu endelevu kwa wadau wake wote ili kuhakikisha sekta ya bima inakua kwa uwazi na kwa manufaa ya wananchi. Ushirikiano na Mahakama ni wa muhimu kwa sababu migogoro mingi ya bima huishia mahakamani, hivyo uelewa wa pamoja utasaidia kulinda haki za wananchi,” amesema.

Ameongeza kuwa ukuaji wa sekta ya bima nchini unahitaji usimamizi madhubuti na uelewa mpana wa sheria, jambo linalofanikishwa kupitia mafunzo hayo.

TIRA imeendesha semina ya elimu ya Sheria ya Bima kwa Mahakimu Wakazi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa lengo ni kuwajengea uelewa mpana kuhusu masuala ya bima na kuongeza ufanisi katika kushughulikia mashauri yanayohusiana na sekta hiyo.

Kupitia semina hiyo, TIRA imelenga kuimarisha ushirikiano na mhimili wa mahakama ili kuhakikisha utekelezaji wa sheria za bima unafanyika kwa ufanisi, uwazi na kwa manufaa ya wananchi.













Matukio mbalimbali katika semina ya utoaji elimu ya sheria ya bima kwa mahakimu wakazi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Picha za pamoja mara baada ya ufunguzi wa semina ya utoaji elimu ya sheria ya bima kwa mahakimu wakazi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...