Gavana wa Anjouan Mhe. Dkt. Zaidou Youssouf ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Comoro Mhe. Azali Assoumani kwa ushirikiano wao wa kipekee ulioiwezesha timu ya wataalamu wa afya kutoka Tanzania kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi wa kisiwa hicho.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kambi maalumu ya matibabu ya kibingwa uliofanyika tarehe 04 Oktoba,2025 Dkt. Youssouf alisema wananchi wa kisiwa hicho wanamchukulia Rais Samia kama Mama yao kutokana na mchango wake mkubwa katika kuboresha afya za wananchi wa Comoro.
“Mama Samia ni mfano wa kuigwa. Siyo tu anapambania maendeleo ya Watanzania, bali pia ya nchi nyingine za Afrika ikiwemo Comoro. Leo tumeshuhudia kwa macho yetu jinsi alivyotuma madaktari wake kuja kuokoa maisha ya wanacomoro wanaokabiliwa na magonjwa mbalimbali”, alisema Dkt. Youssouf.
Aliongeza kuwa serikali yake itaweka utaratibu maalum wa ushirikiano wa kudumu na hospitali za Tanzania, ili wagonjwa watakaohitaji rufaa waweze kupata matibabu nchini humo kwa urahisi zaidi.
“Tutaanza pia kutuma madaktari wetu kwenda Tanzania kwa mafunzo ya kitaalamu na wagonjwa wetu waanze kutumia mfumo wa miadi ya mtandaoni ili wagonjwa kutoka Comoro waweze kuonana na madaktari wa Tanzania bila usumbufu”, aliongeza Gavana huyo.
Aidha, Dkt. Youssouf aliitumia nafasi hiyo kumtakia Mhe. Rais Samia mafanikio katika kampeni za uchaguzi zinazoendelea Tanzania, akisema wananchi wa Anjouan wanamuombea ashinde ili aendelee na kazi yake nzuri ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu aliwapongeza madaktari wa Tanzania kwa kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoyatoa wakati wa ziara yake nchini Comoro alipokutana na wananchi, ambapo alisisitiza umuhimu wa kupeleka huduma za matibabu ya kibingwa kwa wananchi wa kisiwa hicho kabla ya mwaka huu kuisha.
Naye Waziri wa Afya wa Comoro Mhe. Ahamadi Sidi Nahouda alisema kambi hiyo ni ishara ya undugu wa kweli kati ya Tanzania na Comoro, akibainisha kuwa ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 50 tangu nchi hiyo ilipopata uhuru mwaka 1975, kwa kisiwa cha Anjouan kuwa na kambi kubwa ya aina hiyo.
“Tuna zaidi ya wataalamu 50 waliowasili hapa. Hii ni historia mpya kwa taifa letu, tunawashukuru sana kwa moyo wa kujitolea,” alisema Mhe. Nahouda.
Mwenyekiti wa Kamati ya Utalii Tiba Taifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, alisema mwaka jana katika kambi kama hiyo iliyofanyika Ngazidja zaidi ya wagonjwa 2,700 walihudumiwa, baadhi yao walipelekwa Tanzania kufanyiwa upasuaji na wengine wamepona kabisa.
Dkt. Kisenge aliongeza katika kambi hiyo huduma zinatolewa bila malipo huku Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) ikiwa imechangia dawa zenye thamani ya Euro 20,000 zitakazotolewa kwa wagonjwa.
“Tumekuja na vifaa tiba vya kisasa zikiwemo mashine za uchunguzi wa moyo na saratani. Mbali na matibabu, wananchi pia watapewa elimu kuhusu magonjwa yasiyoambukiza. Hadi sasa zaidi ya watu 2,500 wamejiandikisha kupata huduma”, alisema Dkt. Kisenge.
Ushirikiano kati ya Tanzania na Comoro ni ushahidi tosha kuwa Afrika inaweza kujitibu yenyewe kupitia ubunifu, umoja na dhamira ya pamoja ya kulinda uhai wa wananchi wake.




Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kambi maalumu ya matibabu ya kibingwa uliofanyika tarehe 04 Oktoba,2025 Dkt. Youssouf alisema wananchi wa kisiwa hicho wanamchukulia Rais Samia kama Mama yao kutokana na mchango wake mkubwa katika kuboresha afya za wananchi wa Comoro.
“Mama Samia ni mfano wa kuigwa. Siyo tu anapambania maendeleo ya Watanzania, bali pia ya nchi nyingine za Afrika ikiwemo Comoro. Leo tumeshuhudia kwa macho yetu jinsi alivyotuma madaktari wake kuja kuokoa maisha ya wanacomoro wanaokabiliwa na magonjwa mbalimbali”, alisema Dkt. Youssouf.
Aliongeza kuwa serikali yake itaweka utaratibu maalum wa ushirikiano wa kudumu na hospitali za Tanzania, ili wagonjwa watakaohitaji rufaa waweze kupata matibabu nchini humo kwa urahisi zaidi.
“Tutaanza pia kutuma madaktari wetu kwenda Tanzania kwa mafunzo ya kitaalamu na wagonjwa wetu waanze kutumia mfumo wa miadi ya mtandaoni ili wagonjwa kutoka Comoro waweze kuonana na madaktari wa Tanzania bila usumbufu”, aliongeza Gavana huyo.
Aidha, Dkt. Youssouf aliitumia nafasi hiyo kumtakia Mhe. Rais Samia mafanikio katika kampeni za uchaguzi zinazoendelea Tanzania, akisema wananchi wa Anjouan wanamuombea ashinde ili aendelee na kazi yake nzuri ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu aliwapongeza madaktari wa Tanzania kwa kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoyatoa wakati wa ziara yake nchini Comoro alipokutana na wananchi, ambapo alisisitiza umuhimu wa kupeleka huduma za matibabu ya kibingwa kwa wananchi wa kisiwa hicho kabla ya mwaka huu kuisha.
Naye Waziri wa Afya wa Comoro Mhe. Ahamadi Sidi Nahouda alisema kambi hiyo ni ishara ya undugu wa kweli kati ya Tanzania na Comoro, akibainisha kuwa ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 50 tangu nchi hiyo ilipopata uhuru mwaka 1975, kwa kisiwa cha Anjouan kuwa na kambi kubwa ya aina hiyo.
“Tuna zaidi ya wataalamu 50 waliowasili hapa. Hii ni historia mpya kwa taifa letu, tunawashukuru sana kwa moyo wa kujitolea,” alisema Mhe. Nahouda.
Mwenyekiti wa Kamati ya Utalii Tiba Taifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, alisema mwaka jana katika kambi kama hiyo iliyofanyika Ngazidja zaidi ya wagonjwa 2,700 walihudumiwa, baadhi yao walipelekwa Tanzania kufanyiwa upasuaji na wengine wamepona kabisa.
Dkt. Kisenge aliongeza katika kambi hiyo huduma zinatolewa bila malipo huku Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) ikiwa imechangia dawa zenye thamani ya Euro 20,000 zitakazotolewa kwa wagonjwa.
“Tumekuja na vifaa tiba vya kisasa zikiwemo mashine za uchunguzi wa moyo na saratani. Mbali na matibabu, wananchi pia watapewa elimu kuhusu magonjwa yasiyoambukiza. Hadi sasa zaidi ya watu 2,500 wamejiandikisha kupata huduma”, alisema Dkt. Kisenge.
Ushirikiano kati ya Tanzania na Comoro ni ushahidi tosha kuwa Afrika inaweza kujitibu yenyewe kupitia ubunifu, umoja na dhamira ya pamoja ya kulinda uhai wa wananchi wake.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...