Na Andrea Kadege, WAF-Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Ukanda wa Afrika Prof. Mohamed Janabi amesisitiza umuhimu wa ufuatiliaji wa haraka wa wagonjwa na uwekezaji katika mifumo ya afya kama nguzo muhimu ya kudhibiti ugonjwa wa Ebola barani Afrika
Prof. Janabi amesema hayo leo Juni 25, 2026 Jijini Dar es Salaama katika mkutano maalum wa kijadili mustakabali wa kukabiliana na Ugonjwa wa Ebola uliowakutanisha Shirika la Afya Duniani (WHO), Wizara ya Afya na wadau wa maendeleo ambapo Prof. Janabi, alieleza kwa kina mikakati ya kudhibiti ugonjwa wa Ebola, akisisitiza umuhimu wa ufuatiliaji wa haraka wa wagonjwa na uwekezaji thabiti katika mifumo ya afya barani Afrika.
Dkt. Janabi amebainisha kuwa ugonjwa wa Ebola ulitambuliwa kwa mara ya kwanza ncjini DRC, na tangu wakati huo umeendelea kuibua changamoto kubwa za kiafya na kiusalama wa afya ya umma.
Akitaja historia ya milipuko ya awali, amekumbusha mlipuko wa mwaka 2007 katika eneo la Budi Bunya nchini Uganda, ambapo udhibiti wake ulifanikiwa kutokana na uimara wa mfumo wa afya ya umma, na kubainisha kwamba milipuko iliyofuata ilionesha changamoto kubwa zaidi, hasa kutokana na kuchelewa kwa utambuzi wa ugonjwa na mabadiliko ya mwenendo wa maambukizi.
"Moja ya nguzo muhimu katika udhibiti wa Ebola ni ufuatiliaji wa watu waliokutana na wagonjwa (contact tracing), ambapo mafanikio yake hutegemea kiwango cha juu cha ufuatiliaji kinachopaswa kufikia kati ya asilimia 75 hadi 95 na katika baadhi ya maeneo kiwango hicho kimekuwa cha chini, hali inayoongeza hatari ya kuendelea kusambaa kwa maambukizi" amesema Prof. Janabi
Aidha ameeleza kuwa katika baadhi ya matukio, idadi ya watu wanaofuatiliwa inawaweza kuongezeka jambo linaloonyesha ukubwa wa changamoto ya kudhibiti milipuko hiyo akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya nchi, WHO na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha taarifa zinapatikana kwa wakati na hatua za haraka zinachukuliwa.
Kwa upande mwingi amesisitiza kuwa uwekezaji katika sekta ya afya si gharama bali ni uwekezaji wenye manuaa akihimiza kuwa kila hatua ya mapema katika kuzuia milipuko huokoa maisha, hupunguza mzigo wa matibabu na kuimarisha ustahimilivu wa mifumo ya afya barani Afrika.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Ukanda wa Afrika Prof. Mohamed Janabi amesisitiza umuhimu wa ufuatiliaji wa haraka wa wagonjwa na uwekezaji katika mifumo ya afya kama nguzo muhimu ya kudhibiti ugonjwa wa Ebola barani Afrika
Prof. Janabi amesema hayo leo Juni 25, 2026 Jijini Dar es Salaama katika mkutano maalum wa kijadili mustakabali wa kukabiliana na Ugonjwa wa Ebola uliowakutanisha Shirika la Afya Duniani (WHO), Wizara ya Afya na wadau wa maendeleo ambapo Prof. Janabi, alieleza kwa kina mikakati ya kudhibiti ugonjwa wa Ebola, akisisitiza umuhimu wa ufuatiliaji wa haraka wa wagonjwa na uwekezaji thabiti katika mifumo ya afya barani Afrika.
Dkt. Janabi amebainisha kuwa ugonjwa wa Ebola ulitambuliwa kwa mara ya kwanza ncjini DRC, na tangu wakati huo umeendelea kuibua changamoto kubwa za kiafya na kiusalama wa afya ya umma.
Akitaja historia ya milipuko ya awali, amekumbusha mlipuko wa mwaka 2007 katika eneo la Budi Bunya nchini Uganda, ambapo udhibiti wake ulifanikiwa kutokana na uimara wa mfumo wa afya ya umma, na kubainisha kwamba milipuko iliyofuata ilionesha changamoto kubwa zaidi, hasa kutokana na kuchelewa kwa utambuzi wa ugonjwa na mabadiliko ya mwenendo wa maambukizi.
"Moja ya nguzo muhimu katika udhibiti wa Ebola ni ufuatiliaji wa watu waliokutana na wagonjwa (contact tracing), ambapo mafanikio yake hutegemea kiwango cha juu cha ufuatiliaji kinachopaswa kufikia kati ya asilimia 75 hadi 95 na katika baadhi ya maeneo kiwango hicho kimekuwa cha chini, hali inayoongeza hatari ya kuendelea kusambaa kwa maambukizi" amesema Prof. Janabi
Aidha ameeleza kuwa katika baadhi ya matukio, idadi ya watu wanaofuatiliwa inawaweza kuongezeka jambo linaloonyesha ukubwa wa changamoto ya kudhibiti milipuko hiyo akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya nchi, WHO na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha taarifa zinapatikana kwa wakati na hatua za haraka zinachukuliwa.
Kwa upande mwingi amesisitiza kuwa uwekezaji katika sekta ya afya si gharama bali ni uwekezaji wenye manuaa akihimiza kuwa kila hatua ya mapema katika kuzuia milipuko huokoa maisha, hupunguza mzigo wa matibabu na kuimarisha ustahimilivu wa mifumo ya afya barani Afrika.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...