Na Mwandishi Wetu
RAIS  na Mkurugenzi Mkuu wa Octant Energy, Richard Schmitt, amesema Kampuni hiyo bado ina dhamira ya dhati kuendelea kuwekeza nchini kwa kuzingatia sheria viwango vya kitaalamu na maslahi ya wananchi.

Akizungumza katika banda la Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba, Schmitt amesema kampuni hiyo inaendelea kutekeleza shughuli zake kwa kushirikiana kwa karibu na PURA pamoja na wadau wengine.

Akiwa katika banda la PURA, Schmitt amepata elimu kuhusu mfumo wa usimamizi wa shughuli za utafutaji, uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia nchini pamoja na kuhakikisha rasilimali za Petroli zinazoendelezwa zinazingatia sheria, na uwazi.

Octant Energy ni waendeshaji wa Kitalu cha Uchimbaji Tanga ambao wamefika katika banda la PURA kwenye maonesho ya Sabasaba kama moja ya wadau wa PURA. 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...