Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imesema imetumia Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu kwa wadau kuhusu majukumu yake, fursa zilizopo katika sekta ya mbolea pamoja na mnyororo wa thamani wa uagizaji, utengenezaji na usambazaji wa mbolea nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Julai 4, 2026, Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini wa TFRA, Joshua Ng’ondya, amesema mamlaka hiyo imefika kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, umuhimu wa upimaji wa udongo, pamoja na utaratibu wa kujisajili ili kunufaika na mpango wa mbolea za ruzuku.

Amesema kupitia maonesho hayo, wananchi na wafanyabiashara wanapata maelekezo ya namna ya kupata leseni za biashara, kusajili maeneo ya biashara na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa mbolea, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika biashara ya mbolea nchini.

Ng’ondya amesema TFRA ina jukumu la kudhibiti ubora wa mbolea za viwandani na mbolea hai zilizosajiliwa, pamoja na kuhakikisha zinakidhi viwango vinavyotakiwa kabla ya kuingia sokoni na katika mpango wa ruzuku kwa wakulima.

Aidha, ameeleza kuwa mamlaka hiyo inaendelea kutoa elimu kuhusu namna ya kutengeneza, kusajili na kuingiza mbolea sokoni kwa kufuata taratibu zilizowekwa, ili kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora, salama na zenye tija katika kuongeza uzalishaji wa mazao.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...