Vodacom Tanzania PLC imezindua rasmi mashindano ya Gofu ya Vodacom Corporate Masters 2026 kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited yatayofanyika Lugalo Golf Club, ikiwa ni sehemu ya dhamira yake ya kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kukuza ushirikiano na kuleta fursa zenye tija kwa wateja, washirika wa kibiashara na wadau muhimu nchini.
Yakiongozwa na kitengo cha biashara (Vodacom Business), mashindano haya yanatumika kama jukwaa kuu la udhamini wa mchezo wa golf kwa sekta ya biashara, lililobuniwa kuunganisha jumuiya ya wafanyabiashara nchini huku likiimarisha nafasi ya Vodacom kama mshirika wa kuaminika katika teknolojia na huduma za mawasiliano kwa taasisi na mashirika yanayoendelea kukua katika mazingira ya uchumi wa kidijitali.
Mashindano haya yanayotarajiwa kuanza tarehe 1 Agosti 2026, yatawakutanisha wakuu wa makampuni, wafanyabiashara, wataalamu kutoka sekta mbalimbali, wapenzi wa mchezo wa golf pamoja na wateja wa Vodacom ambao watashiriki katika mfululizo wa mashindano hayo pamoja na matukio ya kujenga mitandao ya kibiashara yatakayofanyika kwenye uwanja wa Lugalo Golf Club.
Mpango huu unaakisi dhamira ya Vodacom Business ya kujenga mahusiano yenye thamani yanayovuka mipaka ya biashara za kawaida kwa kutoa jukwaa la ushirikiano, kubadilishana maarifa, ubunifu na kukuza maendeleo endelevu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi alisema mashindano hayo yanadhihirisha dhamira ya Vodacom ya kuimarisha uhusiano wake na jumuiya ya wafanyabiashara nchini Tanzania na ndio maana wameamua kudhamini kwa mwaka wa tatu mfululizo.
"Vodacom tunaamini kuwa ukuaji endelevu wa biashara unajengwa kupitia mahusiano imara na yenye maana. Mashindano ya golf ya Vodacom Corporate Masters 2026 ni zaidi ya mashindano ya michezo, hili ni jukwaa linalowakutanisha viongozi wa biashara, wabunifu na watoa maamuzi ili kujenga uhusiano, kubadilishana mawazo na kusaka fursa mpya zitakazochangia ajenda ya Tanzania ya mageuzi ya kidijitali. Kupitia mpango huu tunaendelea kuziwezesha biashara kwa kutoa suluhisho za teknolojia zenye uhakika huku tukiwapa wateja na wadau wetu uzoefu wa kipekee," alisema Sayi.
Katika kipindi chote cha mashindano hayo, Vodacom Business itaonesha suluhisho zake bunifu za kidijitali zinazojumuisha huduma za mawasiliano, usalama wa kidijitali pamoja na teknolojia za biashara zinazosaidia taasisi kuongeza ufanisi wa shughuli zake, kuharakisha ukuaji na kuendelea kuwa na ushindani katika dunia inayozidi kutegemea teknolojia. Washiriki pia watapata fursa ya kukutana na viongozi wa Vodacom na kupata uelewa wa suluhisho mbalimbali zinazokidhi mahitaji yanayobadilika ya biashara.
Mwenyekiti wa Corporate Masters, Ken Kariuki alielezea mashindano hayo kuwa ni jukwaa la kipekee la ushirikishwaji wa makampuni linalowezesha kuongeza muonekano wa chapa, kujenga mitandao ya kibiashara, kuzalisha fursa za biashara na kuimarisha ushiriki wa wateja.
Tukio hilo la siku moja litashirikisha timu 10 za makampuni zitakazoshindania kombe la Vodacom Corporate Masters 2026, sambamba na eneo maalum la makampuni litaklokuwa na burudani, maonesho mbalimbali, maonesho ya vitu vya kale (vintage) pamoja na eneo maalum la watoto, hivyo kuweka mazingira rafiki kwa familia, kwa washiriki na wageni watakaohudhuria.
Mashindano ya golf ya Vodacom Corporate Masters yanaendelea kudhihirisha dhamira ya Vodacom Tanzania ya kujenga ushirikiano wa kuaminika na kuunga mkono mipango inayozalisha thamani ya kudumu kwa wateja, biashara na jamii. Kwa kuunganisha michezo, biashara na ubunifu, Vodacom inaendelea kuimarisha nafasi yake kama mshirika wa kuaminika katika safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kidijitali.
Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (katikati) akizungumza wakati wa kutangaza udhamini wa Mashindano ya Golf ya Vodacom Corporate Masters 2026, yaliyoandaliwa kwa ushirikiano na Lugalo Golf Club kwa lengo la kuunganisha jumuiya ya wafanyabiashara nchini Tanzania, kuimarisha mahusiano ya kibiashara, kukuza ushirikiano na kuleta fursa zenye tija kwa wateja, washirika wa kibiashara na wadau muhimu nchini. Mashindano hayo yatakayofanyika tarehe 1 Agosti 2026 yanaendelea kuimarisha nafasi ya Vodacom kama mshirika wa kuaminika katika teknolojia na huduma za mawasiliano kwa taasisi na mashirika yanayoendelea kukua katika mazingira ya uchumi wa kidijitali. Uzinduzi huo umefanyika tarehe 16 Julai 2026 jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Katibu wa Corporate Masters, Maryanne Mugo (kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Corporate Masters, Ken Mbaya (kulia).




.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...