Na Karama Kenyunko - Michuzi tv
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeelezwa kuwa Mwenyekiti CHADEMA, Tundu Lissu, hakuwa na ufahamu wa uwepo wa waandishi wa habari katika mkutano wa chama hicho na watia nia uliofanyika Aprili 3, 2025.
Shahidi wa nne wa utetezi, Brenda Rupia, ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, amedai hayo leo Septemba 7, 2026 mbele ya jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru akisaidiana na jaji Fednand Kiwonde na James Karayemaha alipokuwa akitoa ushahidi katika kesi ya uhaini inayomkabili Lissu.
Brenda amedai kuwa, Lissu hakuwa ameandaa mkutano huo wala aliyealika vyombo vya habari, akieleza kuwa jukumu hilo lilifanywa na Sekretarieti ya CHADEMA chini ya Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika.
Amesema yeye ndiye aliyeandika taarifa kwa umma na watia nia kuhusu mkutano huo Machi 27, 2025, na kuiweka katika kurasa za chama kwenye mitandao ya kijamii, huku waandishi wa habari wakialikwa kufanya coverage ya mkutano huo.
Kwa mujibu wa Brenda, takribani watu 250 walihudhuria mkutano huo, wakiwemo watia nia, wajumbe wa Sekretarieti, viongozi wakuu wa CHADEMA pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali, akiwemo Jambo TV.
Brenda amedai Lissu alikuwa mzungumzaji mkuu katika mkutano huo na alitoa hotuba kuhusu msimamo wa chama wa “No Reforms, No Election”, huku akisisitiza kuwa hakumuona akifanya jukumu lingine lolote katika mkutano huo.
Kuhusu maudhui yaliyorushwa na Jambo TV, shahidi huyo amesema yaliyorekodiwa na chombo hicho yalikuwa mali ya Jambo TV na kwamba Lissu hakuwa mfanyakazi wa chombo hicho wala hakuhusika na kurusha matangazo hayo.
Baada ya ushahidi huo, Mahakama iliahirisha kesi hadi kesho saa tatu asubuhi huku Jaji Dustan Ndunguru akieleza kuwa kesi hiyo imeongezewa siku 14 kuanzia leo kwa ajili ya kukamilisha mwenendo wake.
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeelezwa kuwa Mwenyekiti CHADEMA, Tundu Lissu, hakuwa na ufahamu wa uwepo wa waandishi wa habari katika mkutano wa chama hicho na watia nia uliofanyika Aprili 3, 2025.
Shahidi wa nne wa utetezi, Brenda Rupia, ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, amedai hayo leo Septemba 7, 2026 mbele ya jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru akisaidiana na jaji Fednand Kiwonde na James Karayemaha alipokuwa akitoa ushahidi katika kesi ya uhaini inayomkabili Lissu.
Brenda amedai kuwa, Lissu hakuwa ameandaa mkutano huo wala aliyealika vyombo vya habari, akieleza kuwa jukumu hilo lilifanywa na Sekretarieti ya CHADEMA chini ya Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika.
Amesema yeye ndiye aliyeandika taarifa kwa umma na watia nia kuhusu mkutano huo Machi 27, 2025, na kuiweka katika kurasa za chama kwenye mitandao ya kijamii, huku waandishi wa habari wakialikwa kufanya coverage ya mkutano huo.
Kwa mujibu wa Brenda, takribani watu 250 walihudhuria mkutano huo, wakiwemo watia nia, wajumbe wa Sekretarieti, viongozi wakuu wa CHADEMA pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali, akiwemo Jambo TV.
Brenda amedai Lissu alikuwa mzungumzaji mkuu katika mkutano huo na alitoa hotuba kuhusu msimamo wa chama wa “No Reforms, No Election”, huku akisisitiza kuwa hakumuona akifanya jukumu lingine lolote katika mkutano huo.
Kuhusu maudhui yaliyorushwa na Jambo TV, shahidi huyo amesema yaliyorekodiwa na chombo hicho yalikuwa mali ya Jambo TV na kwamba Lissu hakuwa mfanyakazi wa chombo hicho wala hakuhusika na kurusha matangazo hayo.
Baada ya ushahidi huo, Mahakama iliahirisha kesi hadi kesho saa tatu asubuhi huku Jaji Dustan Ndunguru akieleza kuwa kesi hiyo imeongezewa siku 14 kuanzia leo kwa ajili ya kukamilisha mwenendo wake.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...