MOSHI, KILIMANJARO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasihi wananchi wa Mbuyuni, Wilaya ya Moshi, kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo leo, Septemba 1, 2026, wakati akiwasalimia wananchi wa Mbuyuni waliokusanyika kumlaki akiwa katika ziara binafsi mkoani Kilimanjaro.

Amesema kupitia maombi ya wananchi, ataweza kupata hekima na nguvu ya kumsaidia kwa utii Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza majukumu ya kuwatumikia Watanzania.

Mhe. Ndejembi amesisitiza kuwa ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, huku akieleza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi katika kutekeleza majukumu yake.

Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema:

“Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama.”

Amesema kauli hiyo aliitoa pia mkoani Dodoma, kwa wananchi wa Chamwino, mara baada ya kuapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Awali, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambapo alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...