Wakuu wa mikoa wakibadilishana mwenge wa uhuru katika mbio zake mwaka jana. mwasemaje eee wa ughaibuni kuhusu alama hii ya heshima?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. sina mengi kwa hili kwani siujui ni uhuru gani mnaozungumzia hapa. hakuna demokrasia, uvunjwaji wa haki za binadamu uko juu, watu wengine kugeuka miungu watu, umasikini uliokithiri, rushwa inayoshamiri, ubadhirifu kila kukicha, matumizi yasiyeonekana ya kodi...cha ajabu magazeti ya tanzania nayo yamegeuza kibao hayafanyi kazi yake...yaangalie sana ndio chanzo cha vita na migogoro katika jamii. mtaalamu mmoja wa siasa alisema kuwa "AKSANTE NYINGI ZIWAENDEE WANA HABARI KWANI AFRIKA KUSINI ISINGEKUWA NA HAINA TOFAUTI NA NCHI NYINGINE KAMA RWANDA NA BURUNDI KAMA ISINGEKUWA UTEKELEZAJI WA WAJIBU UNAOFANYWA NA WANAHABARI" alisema hivi jinsi ambavyo magazeti hufanyia kazi dukuduku na hisia zoote katika jamii bila kujali makunyanzi ya serekali iliyo madarakani. yalisifiwa hivyo baada ya kufichua madhambi ya Jacob Zuma na kuonyesha vigezo halali vya raisi kumpiga chini, na baada ya hapo kuwakilisha maoni ya makundi yoote katika mgogoro huo bila upendeleo...magazeti ya nyumbani mmekalia habari za kufumaniana na ngono.... na kuwatafutia wenzenu ubaya ili wawapige halafu wasipigiwe kura.....MNA KAZI KUBWA KUFANYA KUJIREKEBISHA...ILI KUINUSURU NCHI.sijui so far ni NOT YET UHURU... tuone sasa awamu hii kama Kikwete atahamasisha uhuru au ataendeleza yale yale!! maana bwana michuzi na wewe si ni mwandishi pia? sijui hili unalionaje unapowaambia watu rudini?

    ReplyDelete
  2. Ungekuwa ughaibuni ningekujibu, ila nashangaa bwana alama kuwa mkosoaji hivyo kaisi hata wamtisha ndesanjo na ida nkya kurejea. yaani unatamka kama hakuna zuri linalofanyika bongo. acha hizo, unakuwa kama mwandishi wa udaku? na hayo magazeti unayosoma wewe yasofichua uozo ni yapi. achana na ya udaku, soma yenye kukamilika kabla hujasema ovyo kama hapo juu. pia kama una 'tip' ya hao wabaya kwa nini usinitonye uone kama tutaacha kuandika.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 16, 2006

    Michuzi,
    unajua ni kawaida ya wanadamu kutorizika. Sasa kama Mark anafikiri Tanznaia hamna demokrasia basi na ende Libya au Saudi Arabia au Congo huko watu wanakochukua silaha na kuwa marais na kuwauwa wenzio wao. Au Mark anataka demokrasia ya Afghanistani ya Mullah Omar?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...