tukiwa na jk wakati huo waziri ya mambo ya nje tukitembelea sehemu zilizokumbwa na mafuriko jimboni kwake chalinze. hii ni katika kuadhimisha posti ya 2000 na ushee katika blogu yenu hii wabongo wote. ashukuriwe/alaaniwe kaka ndesanjo macha kwa kuniambukiza kagonjwa haka ka kublogu...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Michuzi,
    Hii picha bomba sana hata ukiirudia mara elfu moja! Hongera sana kwa kutimiza picha 2000 kwenye blogu yako!

    ReplyDelete
  2. RAIS WA WATU UTAMJUA TU LONG LIVE JK

    ReplyDelete
  3. Michuzi Udereva gani huo,Utazamisha wenzio.

    ReplyDelete
  4. Hongera sana Bwana Michuzi kwa kutimiza picha 2000 kwenye blog,
    kazi unayoifanya ni nzuri sana-inasaidia kutuelewesha na kutupa habari za huko nyumbani. Muhimu zaidi tunaweza kutuma maoni, (ambayo nafikiri huwa yafika mpaka ikulu).
    Nafikiri sasa ni wakati muafaka wa kuitumia hii blog kibiashara-watu 100,000 kwa siku!!!nafikiri wafanyabiashara wanaweza kutumia hii blog kutangaza biashara zao na wewe pia upate chochote-hii kazi kubwa kuifanya bure, usije ukaiua.

    ReplyDelete
  5. Michuzi juzi nilikwambia umezeeka ukabisha! Angalia hapa ulivyokuwa kijana! Sasa ushchuja kaka! Kubali matokeo! Wenzio sisi ndo kwanza kama ma-tineja!

    ReplyDelete
  6. Umetoka mbali michuzi na Kikwete una haki ya kuwa naye kila aendako.Hongera

    ReplyDelete
  7. Michuzi umenimaliza na hii Picha. Huyu Kikwete kweli anajichanganya, nani kiongozi ambaye amesha uonja uwaziri aje kupanda lijiti eti kisa anatathmini mafuriko. Nafikiri ukiitoa kwenye gazeti la daily news uta-waacha wengi hoi. Tafuta namna ya kuiweka basi maana wengi hawataamini macho yao.

    ReplyDelete
  8. Michuzi umechapia, sio Kisarawe ni CHALINZE. rekebisha Caption ya hiyo piche ili iwe sambamba na ukweli wa mambo

    ReplyDelete
  9. Kuna mchizi kwa nyuma ana mche mdomoni nadhani ndio alikuwa navigeta. Hakuna mto karibu wenye mamba au kiboko kweli? Maana angeibuka mamba hapo sijui ingekuwaje!
    Na wewe Michuzi niliwahi kukuuliza je ingetokea mtumbwi ukapinduka, je ungechukua hatua gani? Kuweka kamera sawa ili uchukue picha safi ya mheshimiwa waziri akianguka majini au ungejaribu kutoa msaada na kuacha kamera yako itumbukie majini?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...