hii ni zawadi aliyotaka mshindi wa shindano lilopita, kama anavyosema yeye mwenyewe hapo chini... huyo mwenye kapelo ndo zemarcopolo na hapo ni prague kwenye sherehe za bamboocha


Hallow ndugu Michuzi, habari yako!
Asante kwa kunitangaza mshindi wa shindano lako la kutambua Jengo na mahali lilipo.
Kama ulivyoahidi kwamba, utanipa zawadi ya picha yeyote ile nitakayoiomba, hivyo basi nawakilisha OMBI langu.

Naomba uniwekee ktk blog yako picha ya MJI wa PRAGUE (Czech Republic) ikiwa na Zemarcopolo (original).

Natanguliza shukrani zangu na nasubiri PICHA yangu

Revd. EVM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Haya mzee wa "THE ORIGINAL WOUND HEALERS"nakuona hapo!!
    Naamini muda si mwingi ujao utakabidhiwa kile kitengo cha mifupa "MOI" pale Muhimbili.
    Jamani kwa wasiomfahamu huyu bwana ni "KICHWA TANZANIA ISIKUBALI KUKIPOTEZA"
    1.O-level(Mzumbe- points 7)
    2.A-level(Ilboru-PCB,Students' body President-points 3, na akaongoza Tanzania yote!!
    Keep your head up, Imaan Hamza Kondo!

    ReplyDelete
  2. hongera sana Michuzi kwa hii picha ya huyu Bwana Iman Hamza Kondo ak.a "ZEMARCOPOLO".Picha ni nzuri na washindi nao wamependeza.Mimi nipo Sheffield kaka.
    Iman Kondo tuwasiliane kwa email hii:deogratiusmathew@yahoo.com/mwingereza95@hotmail.com.

    ReplyDelete
  3. twishampoteza, anasoma Czech, basi tena. Akirudi huko MOI watampa mtihani tena, na wanaweza kumkamata pia, mambo ya O au A level ni kukariri tu mjomba.

    ReplyDelete
  4. twishampoteza, anasoma Czech, basi tena. Akirudi huko MOI watampa mtihani tena, na wanaweza kumkamata pia, mambo ya O au A level ni kukariri tu mjomba.

    ReplyDelete
  5. twishampoteza, anasoma Czech, basi tena. Akirudi huko MOI watampa mtihani tena, na wanaweza kumkamata pia, mambo ya O au A level ni kukariri tu mjomba.

    ReplyDelete
  6. Huyo ninani unayemzungumzia Anoni hapo juu Ni Zemarcopolo? Au?.Hii ndio Blogu sasa mzee Zemarcopolo tumekuona live sasa.

    Tunashukuru kukufahamu.

    ReplyDelete
  7. Madoctor wengi wamechoropoka bongo kutokana na kukosa kulipwa kutokana na ujuzi wao.Nawajua madoctor baadhi kama hapo Minnesota wako 3,Australia namjua Dr.Samwel Mwakasendo,Maryland Dr.Nyagawa na wengineo wengi na ni vichwa vizuri sana.Hawa ninaowajua mimi....wako mabingwa wa macho kama Dr.Nyalusi yuko Zimbabwe na Dr.Msuya.Tanzania inabidi iwaangalie hawa madaktari vizuri kama wenzetu ughaibuni.Dr. wa meno USA ana njuru kiama bongo Dr.wa meno ni wa kawaida apart from Dr.Andrew.Tusiwalipe madoctor kama tunavyowalipa polisi au walimu maana hili ni tatizo la dunia nzima polisi au walimu hawalipwi vizuri hata hapa USA.Naanzisha hoja...

    ReplyDelete
  8. Suala la mtihani kwa madaktari walosoma ACCREDITED UNIVERSTIES halipo.Ni INTERNSHIP then kazi mtindo mmoja.

    ReplyDelete
  9. Wewe unayejificha identity yako kuhusu Imaan Hamza Kondo, na kusema eti MAMBO YA O-LEVEL na A-LEVEL NI KUKARIRI TU! Hebu jiulize kwani KUKARIRI unatumia MATAKO AU KICHWA( BRAIN)?

    ReplyDelete
  10. Wewe anon unayesema mambo ya O-level na A-level ni KUKARIRI TU kwani huko KUKARIRI unatumia MATAKO au KICHWA(BRAIN)!

    ReplyDelete
  11. Tz itaendelea kupoteza wataalam wake wengi tu kutokana na sera,maslahi na miundombinu mbofumbofu!viongozi wetu wengi ni makwapukwapu halafu wanakuambia eti wewe mtaalam uache kazi zako za maana ughaibuni ukajenge taifa ambalo wawo wenyewe wanalitafuna kama mchwa!!Hata mazingira ya uwekezaji kwa wale wenye ujasiri yana utata, mtu unaweza kupoteza dola zako bure!Ndio maana wengine hususan wenye familia huku nje huamua kuwekeza hukuhuku maana nchi yetu bongo ni kigeugeu mambo yake mengi hayaeleweki!!

    ReplyDelete
  12. We anaoni wa Sunday, January 21, 2007 11:46:07 PM. Kukariri unatumia kichwa pia, lakini hata kasuku anaweza. Nimeweka jina la huyu jamaa kwa www.pubmed.gov site ambayo ukichwa wa mtu naonekana kwa idadi ya papers alizonazo, na pia journal gani amepublish. hana hata moja huyu. namtakia mafanikio mema.

    ReplyDelete
  13. Kumbe huyu ndio Zermacopolo mwenyewe. Mshiriki mzuri sana wa majadiliano ya maana mtandaoni. Tunashukuru kwa aliyeomba zawadi hii na wewe kuitoa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...