Mr. michuzi naomba nichukue nafasi hii kwa mara nyingine mimi kama mwanafunzi na mwandishi wa barua yangu pepe kwako yenye kichwa cha habari:ZAPOROZHYA STATE MEDICAL UNIVERSITY-UKRAINE “SERIKALI YA TANZANIA MBONA MMETUTELEKEZA?” kukanusha baadhi ya mistari katika barua hiyo kwa kulitumia vibaya katika maelezo yangu jina la mheshimiwa balozi wetu mheshimiwa Chokala na mwakilishi wake ambaye mara kwa mara hutuletea fedha zetu za mikopo kutoka Ubalozini Mr. Francis.
Hii inatokana na jazba ya muda mfupi wakati wa uandishi wa barua hiyo kutokana hali halisi iliyotukuta sisi wanafunzi wa hapa chuoni ila ninakiri kwa hilo kwa kuwa ni watu ambao walikua pamoja na sisi tangu tumewasili hapa Ukraine katika kutusaidia na kutupa moyo mara tu tunapokuwa katika kila wakati mgumu kifedha,hii ni katika kujenga na si kubomoa heshima ya watu hawa muhimu sana ambao tunatambua na kuikubali michango yao katika maisha yetu huku ugenini ila narudia sikuwa na nia mbaya kama ambavyo naweza nikanukuliwa na baadhi ya watu ambao wanaweza wakasoma vipande hivyo vya habari ila ni barua ambayo nilikua nimeiandika nikitegemea dhumuni halisi la barua lifike kwa wahusika nikiomba msaada zaidi kama nilivyokusudia na si kujaribu kuchafua majina ya waheshimiwa hawa muhimu sana kwetu, basi mimi kama binadamu naomba kuchukua nafasi hii kukanusha maelezo hayo na kuwaomba watajwa waheshimiwa hawa kugundua ya kwamba mimi ni mtoto tu kwao kwa hiyo hawana haja ya kukata mikono yao kwa mimi kuichafua tu kwa bahati mbaya
Habari hii naomba iwekwe sehemu kama ile iliyowekwa barua yangu iliyopita kwenye mtandao wako nikionyesha kujirudi kwa kile kibaya nilichokiandika labda kutokana na upeo wangu mdogo kwa waheshimiwa hawa.
Gabu gabu gabu gabu...Chonde chonde kijana.... Wewe ulivyoandika hiyo barua hukukaa chini, ukanywa maji, ukaisoma tena na kujua kuwa wapi ulimi ilikuteleza urekebishe? Wewe ulivyomaliza tu uka click Send Na inaelekea ulikua na hasira sana manake lile lilikua gazeti wala sio barua tena. Sasa baada ya kuisoma mwenyewe tena huku kwenye blog ya Michuzi ndio unaona makosa yako na unataka kujisahihisha.... Kwanza uliwaponza na wenzako hata sijui walikua na habari kuwa majina yao yapo huko pia......Umeshalipua bomu subiri matokeo yake tu kijana.
ReplyDeleteUsitukane wakunga na uzazi ungalipo.
When you loose don't loose the lesson....Just for your info kabla hujajilipua don't say much
we bwege tu! tangu lini hapa pkawa mahali pa kufikishia matatizo yako?!
ReplyDeleteulivyotangaziwa kupelekwa huko taarifa ulizisoma hapa?
pumbafu na nusu.
Kwanza kabisa inabidi uwaombe radhi wao. Kama ulimsoma Shakespeare "She stoops to conquer". Hata hivyo Majuto ni Mjukuu.
ReplyDeleteAcha uwoga kijana!kumbe haufai kuwa kiongozi wa wanafunzi Urusi! inabidi ujiuzulu mara moja.
ReplyDeletewe msomi gani unaandika mambo ya kifala namna hiyo halafu unaanza kula matapishi yako.
ReplyDeleteNyie ndo mnadaiwaga mamilioni ya fidia wa upumbavu wenu, KENGE kabisa wewe!
Mimi nampongeza sana huyo mwandishi (kiongozi wa wanafunzi - Ukraine) kwa ujasiri wake wa kukiri mapungufu yaliyojitokeza.
ReplyDeleteUtamaduni wa kukiri kosa/makosa ni mzuri na unatoa nafasi ya kuanza ukurasa mpya, kwani sisi sote ni wanadamu na makosa hayana mwenyewe!
Natumaini wahusika watapokea ombi lako la msamaha na mtaendelea na ushirikiano.
Yaliyopita si ndwele.......
hahhhahaahahhahahhaah yaaani kicheko hakiniishiii mhhh wewe kijana,nakuonea huruma saana,pole saana kwa yote!usicheze na wakubwa,alaghhhh
ReplyDeleteila jamani msamehen,amekosa! kosa mara ya kwanza sio kosa mbaya kurudia kosa.
USIRUDIE TENA,IWE MWANZO NA MWISHO!
Dhu watu wanaandika hapa yaani basi tu...anyway, Chonde, barua yako ya kwanza inaonesha reaction ya kawaida kwa mtu aliye kasirishwa na kitu fulani hasa ukiwa nje huoni pakujishikiza. Baada ya hasira kupungua umeogopa, pia ni reaction ya kawaida, ila hii ni lesson ya maisha hakuna litakalo kupata wala hao rafiki uliyo weka majina hakuna baya litakalo wapata. Hao waliondika hapo juu wengi hawa elewi maisha mtu unapofikia point mliofikia wakati mko mbali na nyumbani (kiatu usichokivaa...)lakini wasikutishe kama nilivyo sema hapo juu maisha ni shule umejifunza kitu kwa hayo yote. Next time utajua approch gani uchukue, kwa sasa maji yasha mwagika. Do not panic! Aurely
ReplyDeleteKaandika Chokala hii
ReplyDeleteHii ni kali ya mwaka. Kijana katembelewa na wazee wakamtaka kuomba msamaha. Inaonekana vitisho vilikuwa vikali sana. Uandishi wako ni wa ajabu ndio maana unaweza kuandika bila kuangalia ni maneno gani umetumia. Itakuwaje aya hiyo yote uliyoandika hapo juu iwe ni sentensi moja tu? Next time andika halafu uombe msaada watu waipitie kabla hujabandika.
ReplyDeleteyou are trippin bro!! strick with your balls!!!!
ReplyDeleteThe way it seems ni kama bwana Chokala kakulazimisha ukaombe radhi kwa sababu tu yeye ni balozi au kwa sababu tu fedha zenu kila mara zimepitia kwenye mikono yake.Lakini ukweli unabakia palepale kwamba vijana Ukraine mnataabika na watu kama kina Chokala walitakiwa washinikize nyumbani ili msiwe na matatizo kama hayo ugenini.Nina uhakika kabisa atakuwa amekupa vitisho viiingi kwa kawaida ya wakubwa wengi habari zinawekwa upenuni.Ulitakiwa kijana usimamie ukweli 100% bila kuterereka ndivyo wapigania haki wanavyotakiwa kusimama bila kusumbuliwa na vitisho vya hapa na pale.
ReplyDeletewe ni bwege inawezekana hauna matatizo mbona unapayukapayuka kama bata kuwa na uhakika kwanza rudi tanzania isomee ualim bwege we !
ReplyDelete